Joy FM

“Vijana kambi ya wakimbizi Nyarugusu msitumike kuvuruga amani”

10 March 2025, 13:43

Wanawake wakiwa katika maandamano ya siku ya wanawake duniani yalifanyika katika kambi ya wakimbizi nyarugusu

Serikali na mashirika yanayohudumia wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu iliyopo Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma wamewataka vijana kuachana na makundi yanayoweza kuwaingiza katika kufanya vitendo viovu ambavyo vinaweza kusababisha uvunjifu wa amani ndani ya kambi na nje.

Na Tryphone Odace

Vijana wanaoishi katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu wametakiwa kutokubali kutumiwa na makundi yenye nia mbaya Kwa ajili ya uvunjifu wa Amani ndani ya kambi na nje ya kambi hiyo kwani kufanya hivyo watasababisha kutokuwa na Amani katika maeneo ya yao na hata nchi wanapotokea.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa huduma za wakimbizi kutoka wizara ya mambo ya ndani nchini Tanzania Sudi Mwakibasi wakati akizungumza wakimbizi waishio katika kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu Mkoani Kigoma 

Mkurugenzi wa huduma za wakimbizi wizara ya mambo ya ndani nchini Tanzania Sudi Mwakibasi akiwa na baadhi ya viongozi wa kambi na mashirika, Picha na Tryphone Odace

Amesema baadhi ya vijana wamekuwa wakitumika vibaya na watu wenye nia mbaya  Kwa lengo la kuvuruga Amani iliyopo  hivyo kusababisha vitendo vya mauwaji na ukatili kuendelea kuwepo.

Sauti ya Mkurugenzi wa huduma za wakimbizi wizara ya mambo ya ndani nchini Tanzania Sudi Mwakibasi

Hata hivyo Mwakibasi amewataka viongozi wa kidini kuendelea kuhubiri Amani makanisani na kutoa elimu ya usalama kwa vijana na kuwasihi  kuacha vitendo vya ukatili ikiwemo ubakaji na wauwaji.

Sauti ya Mkurugenzi wa huduma za wakimbizi wizara ya mambo ya ndani nchini Tanzania Sudi Mwakibasi

Naye Afisa mwandamizi kitengo cha GBV kutoka UNHCR Rehema Gatega amesema kuwa kuna wajibu mkubwa wa kuhakikisha hakuna vitendo vibaya vinavyoweza kuwakabili wakimbizi wote wanaoishimkatika kambi hiyo.

Sauti ya Afisa mwandamizi kitengo cha GBV kutoka UNHCR Rehema Gatega

Baadhi ya wakimbizi kutoka kambi ya Nyarugusu hasa wanawake  wameomba Serikali na mashirika ya kuhudumia wakimbizi kuweka mikakati madhubuti ya kukabiliana na vitendo viovu wanavyokutana navyo ikiwemo ubakaji hasa wanapoenda kutafuta kuni.

Sauti ya Baadhi ya wakimbizi kutoka kambi ya Nyarugusu
Sauti ya Baadhi ya wakimbizi kutoka kambi ya Nyarugusu, Picha na Tryphone Odace