Joy FM

Mahakama kuu kuleta matumaini mapya kwa wananchi

4 February 2025, 09:24

Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu Tanzania kanda ya kigoma  Agostine  Rwezile ameomba kufanyika kwa marekebisho ya sheria ya hukumu ili kuhakikisha wananchi wanapata haki zao.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu Tanzania kanda ya kigoma  Agostine  Rwezile katikati akiwa katika picha ya pamoja na mawakili.Picha Orida Sayoni

Na Orida Sayon

Amebainisha hayo mapema leo katika maadhimisho ya kilele cha wiki ya sheria yaliyofanyika katika mahakama kuu kanda ya kigoma nakuzindua rasmi shughuli za kimahakama ambapo amesisitiza kufanya utekelezaji wa  hukumu kwa wakati huku kutekeleza hukumu dhidi ya serikali ikiwa miongoni mwa changamoto.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu Tanzania kanda ya kigoma  Agostine  Rwezile

Aidha ametoa rai kwa watumishi wa mahakama na taasisi zinazosimamia haki madai kuzingatia weledi ,uadilifu na uwajibikaji wa majukumu yao huku akiwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa watumishi wa maswala ya utatuzi wa migogoro kusaidia upatikanaji wa haki kwa wakati

Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu Tanzania kanda ya kigoma  Agostine  Rwezile

Akitoa risala kwa mgeni rasmi wakili wa serikali mwandamizi Geoge Kalenda  kwa niaba ya mwanasheria mkuu wa serikali amesema katika kuendea safari ya Tanzania  ya 2050 taasisi zinazosimamia haki madai zinapaswa kuwa nyenzo ya kuifanya Tanzania kufikia uchumi wa kati na kuzingatia haki, na utwala bora na kisheria.

Wakili wa serikali mwandamizi Geoge Kalenda

Baadhi ya wananchi walihudhuria katika maadimisho hayo akiwemo msaidizi wa kisheria kutoka Paralega organization wakawa na kusema juu ya utendaji wa shuguli za kimahakama na ushirikiano wao kwa mahakama.

Wananchi