Joy FM

Wakristo watakiwa kuliombea taifa amani Kasulu

23 September 2024, 13:26

Waumini kutoka makisa yote 10 alipohudumu mchungaji Ndenza, Picha na Emmanuel Mamangu

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mji wa Kasulu amewataka wakristo kuendelea kuliombea taifa na mshikamano hasa katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27 mwaka huu.

Na Emmanuel Kamangu – Kasulu

Waamini wa kanisa la Anglikana wilayani Kasulu wametakiwa kuendelea kuwaombea  wachungaji wastaafu ili waendelee kuwa na ari ya kumtumkia Mungu kwa moyo wao wote.

Ameeleza hayo Mwenyekiti wa Halamashauri ya Mji wa Kasulu Bw. Noel Hanula akiwa  mgeni rasmi  kwa niaba ya Mkurugenzi wa Bwami hotel Dubai Chocha katika hafla ya kumuaga mchungaji  Amon Ndenza wa Kanisa la Anglikana Parishi ya Mwanga Msanga wilayani Kasulu na kumpongeza mchungaji Ndeza kwa utumishi wake mwema huku akiwaomba  viongozi wa dini  kuiombea Tanzaia ili iendelee kuwa na amani na utulivu hasa kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa hapo Novemba mwaka huu.

Sauti ya Mwenyekiti wa halamashauri ya mji wa kasulu Bw. Noel Hanula

Mchungaji Ndeza amehudumu katika utumishi  wake kwa takribani miaka 39 akishirikiana kwa ukaribu na mama mchungaji  Bi Leonita Mahobe wamesimulia safari ya utumishi wao ambayo ilikuwa ya neema huku wakiwashukuru waamini kwa kuwatia  moyo wakati  wote mpaka kufika sasa wanapo staafu.

Sauti ya mchungaji  Amon Ndenza wa Kanisa la angrikani Parishi ya mwanga

Kwa upande wao wamini wa kanisa la angrikani  wamesema  mch ndenza katika huduma yake ya utumishi amekuwa mtu wa haki na  mwenye upendo huku wakimuombea afya njema.

Sauti ya wamini wa kanisa la angrikani  wamesema  Mch ndenza

Aidha Mkurugenzi wa kanda ya heru juu Mch, Pison Elia  akiwa katika hafla hiyo amesema mchungaji ndenza kila alipo pita kufanya huduma ameacha alama kubwa kwa kuwaletea waamini maendeleo ya kiroho na kimwili.

Mchungaji Amoni ndenza akishukuru waamini wa angrikani wa mwanga msanga na Anglikani mchungaji mwema mrusi katika falfa ya kustafu.