Joy FM

Serikali yatumia bilioni 19 kuboresha sekta ya afya Kigoma

19 September 2024, 10:39

Mkuu wa Mkoa Kigoma Kamishna mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji, Thobias Andangenye, Picha na Jamse Jovin

Serikali imesema kuwa itaendelea kujenga na kuboresha miradi mbalimbali hususani miradi ya afya kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi na kupata huduma karibu na maeneo yao.

Na James Jovin – Kibondo

Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita serikali imefanya uwekezaji wa Zaidi ya shilingi bilioni 19 katika sekta ya afya kwa mkoa wa Kigoma pekee ikiwa ni mkakati wa kuboresha huduma za afya na kupunguza vifo vitokanavyo na ukosefu wa dawa muhimu na vifaa tiba.

Hayo yamebainishwa na naibu waziri wa wizara ya Tamisemi bi. Zainabu Katimba wakati wa ziara ya naibu waziri mkuu na waziri wa Nishati Dr. Dotto Biteko katika wilaya ya Kibondo.

Sauti ya Naibu waziri wa wizara ya Tamisemi Bi. Zainabu Katimba

Aidha mbunge wa jimbo la Muhambwe Dr. Frolence Samizi amesema kuwa wilaya ya Kibondo imefunguliwa katika miundo mbinu mbali mbali hasa ujenzi wa madarasa ya shule za msingi na sekondari hivyo kuinua taaluma kwa kiasi kikubwa.

Sauti ya mbunge wa jimbo la Muhambwe Dr. Frolence Samizi

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye ameipongeza serikali kupitia kwa raisi samia kwa kazi kubwa waliyoifanya hasa katika mkoa Kigoma kwa kufungua miundo mbinu ya barabara zilizokuwa tatizo kubwa ndani ya mkoa huo.

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye

Nae naibu waziri mkuu na waziri wa nishati Dotto Biteko amesema kuwa serikali inaendelea kufanya kazi kubwa ya kujenga miundo mbinu na uchumi wa nchi hivyo kila mmoja anapaswa kuunga mkono juhudi za serikali na si kubeza maendeleo yaliyopo.

Sauti ya Naibu waziri mkuu na waziri wa nishati Dotto Biteko