Joy FM

Waziri wa Uvuvi azindua kiwanda cha kuchakata mazao ya uvuvi

16 August 2024, 15:00

Waziri wa uvuvi Abdallah Ulege akizindua kiwanda cha kuchakata mazao ya uvuvi, Picha na Lucas Hoha

Serikali imesema kuwa itaendelea kuweka mazingira bora kwa wawekezaji wa ndani na nje ili waweze kufanya kazi katika mazingira rafiki.

Na Lucas Hoha – Kigoma

Waziri wa mifugo na Uvuvi nchini Abdallah Ulega amewahakikishia wananchi wa mkoa wa kigoma kuwa serikali imedhamiria kwa dhati kuufungua mkoa huo kuwa lango la biashara katika sekta mhimu ikiwemo kujenga viwanda vya uvuvi ili wananchi kujikwamua kiuchumi.

Mh. Ulega ameyasema hayo wakati akiweka jiwe la msingi kwenye viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi ikiwemo kiwanda Cha Mkuyu Fish Export kilichopo kata ya kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Waziri wa uvuvi Mh. Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa Kigoma, Picha na Lucas Hoha

Amesema ujenzi wa viwanda hivyo itasaidia vijana kupata ajira.

Sauti ya Waziri wa mifugo na Uvuvi nchini Abdallah Ulega

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa kigoma Kamishina jenerali mstaafu wa jeshi la zimamoto na uokoaji Thobias Andengenye mkuu wa wilaya ya Kigoma Salum Kalli amesema uongozi wa mkoa wa kigoma utatoa ushirikiano kwa wawekezaji huku akitaja baadhi ya mambo mhimu ambayo yamefanywa na serikali ikiwemo kujenga barabara, uboreshaji wa uwanja wa ndege na uboreshwaji wa hospitali.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Kigoma Salum Kalli

Kwa upande wao baadhi wa viongozi ambao wamewekeza viwanda vya uchakataji wa mazao ya Uvuvi wameomba serikali kupunguza Kodi na kulinda rasilimali za ziwa Tanganyika Ili samaki wapatikane muda wote.

Sauti ya baadhi wa viongozi ambao wamewekeza viwanda vya uchakataji wa mazao ya Uvuvi