Joy FM

Wananchi wamlilia Mchengerwa migogoro ya ardhi

15 August 2024, 08:27

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa, Picha na Kadislaus Ezekiel

Serikali imesema itaendelea kushirikiana na wananchi ili kubaini na namna ya kutatua migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikisababisha maafa kwa wananchi hususani wafugaji na wakulima nchini.

Na Kadislaus Ezekiel – Kasulu

Wananchi katika kata ya Kagerankanda wilayani Kasulu mkoani Kigoma, wamelalamikia  serikali kuchukua ardhi ya kilimo katika eneo la msitu wa akiba makere kusini,  kwa kudai eneo hilo walikuwa wakilitumia kwa shughuli za Kilimo, ambapo wamemuomba Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa kusaidia utatuzi wa changamoto hiyo.

Ni wakuu wa wilaya za mkoa wa Kigoma wakiwa katika mkutano na waziri wa Tamisemi Mchengerwa

Wakiwa katika mkutano na viongozi wa mkoa pamoja na Waziri wa Tamisemi Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa, wananchi wamesoma risala ya kijiji na kuomba serikali kurudisha ardhi ambayo wanadai ilichukuliwa bila makubaliano na kukosa sehemu za kilimo.

Sauti za wananchi wa kata ya Kagera Nkanda wilayani Kasulu

Hatua hiyo ikamfanya Waziri Mchengerwa kumtaka mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Izack Mwakisu kutoa ufafanuzi juu ya suala hilo.

Sauti ya Mkuu wa wilaya Kasulu mkoani Kigoma

Kisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa akieleza hatua za kuchukua kumaliza mgogoro huo kwa kushirikiana na wizara ya ardhi.

Sauti ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa.