Joy FM

Ukatili unavyowatesa kisaikolojia wanawake Kigoma

14 August 2024, 14:22

Wanawake wakiwa katika picha ya pamoja, Picha na Mtandao

Licha ya serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani Kigoma kuungana na kutoa elimu ya masuala ya ukatilii, bado unyanyasaji wa wanawake kwenye familia umeendelea kuacha simanzi, makovu na huzuni miongoni mwao kwa vipigo ndani ya familia.

Na Ntezimana Gervas – Kigoma

Wanawake mkoani Kigoma wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu ya masuala ya ukatili wanaofanyiwa majumbani hasa waliopo kwenye ndoa hususani kipigo ili kuweza kupunguza baadhi ya athari katika ndoa ikiwemo kusambaratika kwa familia.

Wakizungumza na Radio Joy FM, wanawake hao wameeleza kuwa wanapofanyiwa ukatili wanapata athari kubwa zinazosababisha kutofanya  shughuli zao  jambo linalosababisha  kurudi nyuma kiuchumi na kuwaathiri kisaikolojia.

Sauti ya wanawake wakieleza madhila wanayopitia ndani ya familia kwa kunyanyaswa

Nao baadhi ya wanaume wameeleza sababu zinazowafanya kutekeleza vitendo vya ukatili ikiwemo baadhi ya wanawake kushindwa kutimiza majukumu yao.

Sauti za wanaume wakizungumzia ukatilii kwa wanawake

Bw. Rajabu Issa ambaye ni mwakilishi wa Shirika la BACKAIDS, amesema kuwa wanajitahidi kutoa elimu kwa wanawake juu ya kuwaeleza mbinu mbalimbali za kujiepusha na masuala yanayoweza kupelekea kufanyiwa ukatili.

Sauti ya mwakilishi wa shirika la BackAids

Kwa upande wake, Mkuu wa Dawati la Jinsia manispaa  ya Kigoma Ujiji, Jackline Gabriel ameeleza kuwa elimu inaendelea kutolewa katika jamii kuhusu ukatili huku akiitaka jamii kutoa taarifa za vitendo hivyo.

Sauti ya Mkuu wadawati la jinsia manispaa ya kigoma ujiji