Joy FM

Ziwa Tanganyika kufunguliwa rasmi Agosti 15

14 August 2024, 13:58

Muonekano wa Ziwa Tangnayika ambalo linaelekea kufunguliwa baada ya shughuli kufungwa ndani ya ziwa hilo, Picha na Tryphone Odace

Serikali iliamua kuchukua uamzi wa kufunga Ziwa Tanganyika na shughuli za uvuvi ili kupisha mazalia ya samaki kuongezeka kutokana na kwamba uvuvi haramu umekuwa ukiathiri ukuaji wa samaki ambao wanavuliwa kiharamu.

Na Lucas Hoha – Kigoma

Wakati shughuli za uvuvi zikiwa zinaelekea kufunguliwa katika ziwa Tanganyika, Mkurugenzi wa Uvuvi  nchini Prof. Mohammed Shekhe amewaagiza wavuvi kutumia kanuni na sheria za uvuvi ili kuepuka uharibifu wa mazalia ya samaki kwa mara nyingine.

Doria maalum ya ukaguzi ndani ya Ziwa Tanganyika iliyofanywa na mkurugenzi wa uvuvi nchini pamoja na viongozi wengine akiwemo mhifadhi wa Ziwa Tanganyika Agnely Lishela zikiwa zimesalia siku mbili tu shughuli za uvuvi kuanza upya.

Muonekano wa samaki aina ya mgebuka wanaovuliwa Ziwa Tanganyika, Picha na Tryphone Odace

Mkugenzi huyo amewatoa hofu wananchi na wavuvi kuwa serikali ilifunga ziwa hilo kwa nia njema nakuwa hawatarajii kuona wavuvi wanakiuka kanuni na sheria za uvuvi.

Sauti ya mkurugenzi wa uchaguzi nchini tanzania

Kwa upande wake Mhifadhi wa Ziwa Tanganyika Agnely Lishela amesema, katika kipindi ambacho shuguri za uvuvi zilikuwa zimefungwa hakuna wavuvi ambao wamekamatwa wakivua  kihole, huku akiwatoa hofu wananchi wa mkoa wa kigoma kuwa serikali haijaongeza siku za kulifunga ziwa hilo.

Sauti ya mhifadhi wa ziwa tanganyika

Shughuri za uvuvi katika Ziwa Tanganyika zilifungwa  kwa muda wa miezi 3 tangu may 15 mwaka wa 2024 kwa  lengo la kuacha samaki kuzaliana na kuongeza mazao yatokanayo uvuvi ndani ya ziwa hilo na sasa linafunguliwa  Augost 15 mwaka huu ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa waziri wa mifungo na uvuvi  Abdallah Alega.