Joy FM

Wadau watakiwa kusaidia kuboresha miundombinu ya elimu

7 August 2024, 12:04

Ezra Mikamba mdau wa maendeleo ambaye akizungumza mara baada ya kutoa msaada wa komputa, Picha na Emmanuel Kamangu

Serikali wilayani kasulu mkoani kigoma imewataka wadau wa maendeleo kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha miundombinu ya elimu ili kuhakisha wanafunzi wanapata elimu bora.

Na Emmanuel Kamangu – Kasulu

Wadau wa maendeleo wilayani Kasulu  wameaswa kuendelea kumuunga mkono Raisi Dkatari samia suruhu hasani katika kuhakikisha shule za msingi zinakuwa na miundombinu ya kutosha ya  Tehama ili kuongeza ufaulu mashuleni.

Ameeleza hayo mdau wa maendeleo Bw, Ezra Mikamba wakati akikabidhi komputa mbili moja kwa shule ya msingi nyankole na nyingine kwa shule ya msingi titye zote zikiwa ni shule za kata ya titye na lengo ikiwa ni kuwasaidia walimu kuchapa mitihiani ya mazoezi shuleni na  kuondokana na garama za kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za stationari

Wanafunzi waliopatiwa msaada wa komputa, Picha na Emmanuel Kamangu
Sauti ya mdau wa maendeleo Bw, Ezra Mikamba

Kwa upande wake Mratibu Elimu kata ya titye Bw, Yoabu Hinyula amewaomba walimu kutumia komputa hizo kutoa majaribio ya kutosha kwa wanafunzi jambo litakalo saidia kuongeza ufaulu katika mitihani ya Taifa.

Sauti ya Mratibu Elimu kata ya titye Bw, Yoabu Hinyula

Aidha mwalimu wa Talumu shule ya msingi titye Bw. Gabriel Magarya pamoja na mkuu wa shule ya msingi nyankole Bw,Jaktan Nyakimwe kwa pamoja wamemshukuru Bw, Mikamba kwa msaada huo kwani utasaidia kuondokana na adha ya kuchapisha mitihani nje na shule zao.

Sauti ya mwalimu wa Talumu shule ya msingi titye Bw. Gabriel Magarya pamoja na mkuu wa shule ya msingi nyankole Bw,Jaktan Nyakimwe

Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi titye na nyankole mmoja wao akiwa Malaki Leonadi wamesema komputa hizo  ni nyenzo bora ya kusoma kwa vitendo somo la tehema na kuongeza ufaulu katika somo hilo.

Mmoja wa wanafunzi wakitoa shukrani baada ya kupata msaada wa kumputa, Picha na Emmanuel Kamangu