Joy FM

NGO’s zatakiwa kuweka uwazi kwenye miradi

17 July 2024, 13:17

Katibu tawala wa wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtewele

Serikali imesema itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa mashirika yasiyo ya kiserikali ili yaweze kufanya kazi katika mazingira bora.

Na Hagai Ruyagila – Kasulu

Mashirika yasiyo ya kiserikali yametakiwa kuongeza uwazi katika utendaji wao wa kazi ili serikali ijuwe namna wanavyotekeleza miradi yao ya maendeleo katika jamii kuliko kufichaficha.

Hayo yameelezwa na katibu tawala wa wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtewele wakati akimuwakilisha mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanal Isaac Mwakisu katika kikao cha pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali cha kujadili taarifa za utekelezaji robo ya nne ya mwaka 2023/2024 ndani ya ukumbi wa halmashauri ya Mji Kasulu.

Baadhi ya wadau wa mashirika yasiyo ya kiserikali wakiwa katika mkutano wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, Picha na Hagai Ruyagila

Bi, Mtewele amesema serikali inahitaji kujua mapato yanayoingia na kutoka katika mashirika hayo na namna wanavyotumia fedha hizo na endapo watafanya kazi kwa kuficha haitakuwa jambo zuri.

Sauti ya katibu tawala wa wilaya ya Kasulu Bi. Theresia Mtewele

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu Dkt Semistatus Mashimba ameyasisitiza mashiurika hayo kuongeza nguvu kwenye suala la kilimo huku Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye akiwaomba kuendelea kufanya kazi kwa pamoja ili kuleta chachu ya maendeleo katika halamashauri zote mbili.

Sauti ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu Dkt Semistatus Mashimba

Nao baadhi ya wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali yaliyohudhuria kikao hicho wamesema ni vizuri kufanya kazi zao kwa uwazi huku wakiishirikisha serikali maana mashirika mengine yanaweza kufanya kazi kinyume na sheria na maadili ya kitanzania.

Sauti ya wawakilishi wa mashirika yasiyo ya kiserikali

Kikao hiki ni cha pamoja cha mashirika yasiyo ya kiserikali kujadili taarifa za utekelezaji robo ya nne ya mwaka 2023/2024 ndani ya ukumbi wa halmashauri ya Mji Kasulu.

Washirika wa kikao cha mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, Picha na Hagai Ruyagila