Joy FM

Dkt. Mpango amkalia kooni mkandarasi anayejenga barabara ya Buhigwe -Kasulu

10 July 2024, 16:00

Makamu wa rais wa jamhuri ya muungano wa tanzania Dkt. Philip Mpango,Picha na OMR

Wizara ya ujenzi kupitia kwa waziri wake Innocent Bashungwa ametakiwa kuhakikisha kumsimamia mkandarasi anajenga barabara ya Buhigwe hdi Kasulu ili iweze kukamilika kwa wakati.

Na Josephine Kiravu – Buhigwe

Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philip Mpango  amemtaka Mkandarasi anayejenga barabara ya Kasulu- Buhigwe, Manyovu kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo ifikapo Machi 2025 kwani Kukamilika kwa Barabara hiyo ambayo ni sehemu ya ujenzi wa bararaba ya Kabingo-Kasulu hadi Manyovu yenye urefu wa Km.260.6 

Akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Buhigwe, Mhe. Dkt. Mpango  amesema  maendeleo ya mkoa yamechelewa kutokana na  kutokuwepo kwa miundombinu bora ya barabara, umeme na huduma nyingine za kijamii hivyo wananchi mkoani hapa wanapaswa kutumia fursa ya kukamilika kwa huduma hizo kujiimarisha kimaendeleo.

Sauti ya Makamu wa rais wa Jamhuri ya muunganowa tanzania

Upande wake Waziri wa Ujenzi Inocent Bashungwa amemuhakikishia Makamu wa Rais kuwa barabara ya Kasulu Manyovu  itakamilika ifikapo Machi 2025 ili kuruhusu wananchi kuitumia na kuondokana na adha wanazozipata kutokana na kutokamilika kwa barabara hiyo.

Waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa
Sauti ya Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa

Aidha katika hatua nyingine akitoa  ufafanuzi  kuhusu hali ya usambazaji wa Nishati ya Umeme wilayani Buhigwe, Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga amesema jumla ya vijiji 107 havina umeme, ambapo vijiji 97 mkandarasi yupo kazini na vingine 14 vipo katika hatua ya kufanyiwa Tathmini.

  Amesema Wizara kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamefanikiwa kuvifikia vijiji vyote wilayani humo japo utekelezaji wa kazi ya kuweka umeme hufanyika kwa awamu kuendana na Bajeti inavyopangwa na serikali.