Joy FM

Dkt. Mpango aelekeza barabara ya Malagarasi -Uvinza kukamilika kwa wakati

9 July 2024, 09:04

Makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Philip Mpango, Picha na Josephine Kiravu

Serikali imesema inaendelea na utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini ikiwemo barabara na umeme ili kuhakikisha mkoa wa kigoma unafunguka na kuwa kitovu cha biashara kutokana na kupakana na nchi za Congo na Burundi.

Na Josephine Kiravu

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Philip Isdor Mpango amemtaka waziri wa Ujenzi kuhakikisha anamsimamia mkandarasi anaetekeleza ujenzi wa barabara ya Malagarasi-Ilunde-Uvinza anakamilisha kwa wakati.

Makamu wa Rais ametoa maelekezo hayo akiwa ziarani wilayani uvinza Mkoani Kigoma ambapo  ameanza ziara yake kwa kufanya ukaguzi wa maendeleo ya miradi mbalimbali ya maendeleo mbapo amesema kukamilika kwa barabara hiyo kutasaidia kufungua mkoa wa kigoma na mikoa mingine lakini na nchi jirani ikiwemo Burundi na Congo.

“tumetembea kwenye vumbi kwa muda mrefu sana nikuombe waziri wa ujenzi simamia ujenzi wa barabara hiii ikamilike ili wananchi wasipate usumbufu kwenye kusafirisha bidhaa zao dhamira ya rais ni kuona wananchi wanapata huduma bora”

Sauti ya makamu wa rais wa Tanzania Dkt. Mpango

Na hapa Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa anaeleza hatua zilizofikiwa na matarajio ya kukamilika kwa mradi huo wa barabara.

Waziri wa ujenzi Mh. Innocent Bashungwa, Picha na Josephine Kiravu
Sauti ya waziri wa ujenzi Innocent Bashungwa

Hata hivyo mbali na kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo Makamu wa Rais amezungumza na kusikiliza kero za wananchi wa Uvinza pamoja na kuweka jiwe la msingi kwenye kituo Cha kupoza umeme katika eneo la Kidahwe.

Ni wananchi wa Uvinza wakiwa katika mkutano wa hadhara wakati Makamu wa rais akizungumza nao, Picha na Josephine Kiravu

Makamu wa Rais ataendelea na ziara yake ya kikazi kwa kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa upanuzi wa uwanja wa ndege Kigoma.