Joy FM

Zaidi ya shule 9 Uvinza zina uhaba wa madawati 1,000

2 July 2024, 15:57

Shule za msingi katika kata ya Ilagala wilyani uvinza zinakabiliwa na uhaba mkubwa madawati hali inayopelekea wanafunzi kukaa chini.

Wananchi wa kata ya Ilagala wilayani Uvinza mkoani Kigoma wameomba serikali kuwasaidia kupunguza tatizo la madawati linazozikubwa shule za kata hiyo ili kuwasaidia watoto kuondokana na tatizola kukaa chini

Na Kadislaus Ezekiel – Uvinza

Shule za msingi zaidi ya tisa katika kata ya Ilagala wilayani Uvinza mkoani Kigoma, zinakabiliwa na uhaba wa madawati zaidi ya elfu moja, hali inayosababisha wanafunzi wengi kusoma wakiwa wamekaa chini na kuwa kikwazo katika ujifunzaji na ufundishaji.

Baadhi ya wazazi wakizungumzia suala la ukosefu wa madawati, wakati wa uzinduzi wa kukabidhi madawati miatatu, kwa shule za msingi za kata ya Ilagala, ambazo zimetolewa na  mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi ilagala na mdau wa maendeleo thadeo ndenzako wameomba serikali na wadau wengine kusaidia upatikanaji wa madawati ya kutosha.

Sauti ya wananchi wa ilagala wakiwa wanalalamikia ukosefu wa madawati

Mdau wa maendeleo Thadeo Ndenzako amesema atakabidhi madawati miatatu kwa shule zote za kata ya ilagala ili kusaidia watoto kuepuka kukaa chini wakiwa shule.

Sauti ya mdau wa maendeleo aliyetoa madawati

Kaimu mratibu elimu kata, kata ya ilagala jonathan mayane amesema shule zote za kata zinaupungufu wa madawati zaidi ya elfu moja ili kukidhi mahitaji ya wanafunzi, wakati mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Uvinza Dinnah Mathamani, katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania Chama Cha Mapindu mkoa wa Kigoma Sarah Kairanya amesema atahakikisha saula hilo linafanyiwa kazi mara chini ya Tamisemi ili kusaidia wananafunzi.

Sauti ya mratibu elimu kata, kata ya Ilagala Jonathan Mayane