Joy FM

TASAF yageuka neema kwa kaya masikini

28 May 2024, 10:31

Baadhi ya wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini wilayani kibondo mkoani kigoma, Picha na James Jovin

Serikali wilayani kibondo mkoani kigoma imesema mpango wa kunusuru kaya masikini umesaidia kaya nyingi kujinusuru na umasikini kupitia elimu ya namna ya kutumia fedha wanazopewa katika kuzalisha mali ikwemo ufugaji.

Na James Jovin – Kibondo

Baadhi ya kaya masikini katika kijiji cha Kumkugwa wilayani kibondo mkoani kigoma wamesema kuwa wamenufaika na mradi wa TASAF kiasi cha kuweza kujenga nyumba za bati, kusomesha watoto shule na kufuga mifugo

Wamebainisha hayo wakizungumza na radio Joy wakati wakipewa mafunzo ya namna bora ya kujikwamua na lindi la umasikini ili mradi huo wa TASAF utakapoisha waweze kuendelea na maisha kama kawaida

Bi. Elizabeth Kabika pamoja na bi. Godberter Fransisco ni miongoni mwa wanufaika wa tasafu katia kijiji cha Kumkugwa wilayani Kibondo na hapa wanaelezea jinsi walivyonufaika na kujikwamua katika lindi la umasikini.

Sauti ya wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini kibondo

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Kumkugwa bw. Damian Gwimo ameitaka serikali kuendelea kuwajali wananchi hasa wanaoishi katika mazingira magumu ili kuwakwamua katika lindi la umasikini na kuleta maendeleo endelevu miongoni mwa jamii.

Sauti ya mwenyekiti wa kijiji cha kumkugwa wilayani kibondo

Nae mratibu wa TASAF wilayani Kibondo bw. Dotto Makunja amesema kuwa katika wilaya ya Kibondo zaidi ya kaya elfu kumi zimenufaika na mradi wa kunusuru kaya masini TASAF ambapo wameweza kujikwamua katika matatizo mbali mbali na kukidhi mahitaji ya msingi katika maisha ya kila siku. 

Sauti ya mratibu wa tasaf wilayani kibondo