Joy FM

DC Kigoma ahimiza waumini kujiandikisha daftari la mpiga kura

27 May 2024, 14:36

Mkuu wa wilaya Kigoma Salum Kalii katikati akiwa na viongozi wa kanisa la EAGT Mwasenga, Picha na Prisca Kizeba

Wakati zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura likitarajiwa kuzunduliwa julai mosi mwaka mkoani kigoma, viongozi wa dini na wadau mbalimbali wametakiwa kuhimizi waumini na jamii kwa ujumla kujitokeza kujiandikisha kwenye zoezi hilo la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura.

Na Prisca Kizeba – Kigoma

Mkuu wa Wilaya Kigoma Mh. Salum Kalli amewataka viongozi wa dini ya kikristo Mkoani Kigoma  kuwahiza waumini wao kujitokeza kujiandikisha katika  zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura ambalo linatarajiwa kuznduliwa mwanzoni mwa mwezi Julai mwaka huu mkoani hapa.

Mh. Kalli amesema hayo wakati akizungumza na  waumini wa  kanisa la (EAGT) Mwasenga ambapo amesema kuwa viongozi wa Dini ni chachu kubwa ya kuhimiza watu kujitokeza kujiandikisha katika daftari la mpiga kura.

Sauti ya mkuu wa wilaya kigoma Salum Kalli
Baadhi ya viongozi wa kanisa la EAGT mwasenga wakiwa na mkuu wa wilaya kigoma Salum Kalli, Picha na Prisca Kizeba

Aidha Mh. Mkuu wa wilaya Kigoma amesema  ni lazima waumini wasimame katika imani na kuendelea kuliombea taifa ili kudumisha amani.

Sauti ya mkuu wa wilaya kigoma salum kalli

Kwa upande wake,  Mkuregenzi msaidizi wa utafiti wa sayansi ya mistu kutoka taasisi ya Jane Goodal Dkt Zabibu  Kabalika  ameiomba jamii kuona umuhimu wa kutunza mazingira ili kudhibiti hali ya mabadiliko ya tabii ya nchi.

Sauti ya mkurugenzi msaidizi wa utafiti wa sayansi ya misitu Janegoodal

Naye mchungaji wakanisa hilo Agustino kizeba ambaye pia ni Mwenyekitiu Msaidizi  wamakanisa ya Kipetekoste (CPCT) amemuahidi Mkuu wa Wilaya  kuwa  atawahimza waumi pamoja viongozi wote wa dini kujtikeza katika kujiandikisha katika zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la mpiga kura ambalo linatarajiwa kuzinduliwa mwezi julai.

Sauti ya mchungaji wa kanisa la EAGT mwasenga

Hata hivyo badhi ya waumini waliohudhuria ibaada hiyo wakaeleza.

Sauti ya waumini wa kanisa la EAGT mwasenga Manispaa ya Kigoma Ujiji