Joy FM
Joy FM
9 April 2026, 17:09

Matumizi ya chupa zilizotumika kufungashia vyakula si salama kwa sababu yanaweza kusababisha magonjwa ya tumbo, sumu mwilini, na madhara ya muda mrefu kiafya.
Na Emmanuel Kamangu
Wanaotumia maziwa, asali, juisi na mafuta ambayo hutunzwa katika vifungashio vya chupa za plasitiki zilizokwisha kutumika wako hatarini kukumbana na magonjwa mbali mbali hasa magonjwa ya tumbo.
Kumekuwa na wimbi kubwa la wajasiliamali na baadhi ya wafanyabiashara kufunga vitu mbali mbali katika Chupa zilizokwisha kutumika hasa chupa za maji na soda jambo linalotajwa ni hatari kwa afya ya mlaji..
Akizungumza na Redio Joy Fm, Mratibu wa huduma za shirika la Viwango Tanzania TBS katika halmashauri ya mji wa kasulu Bw. Gribeti mosh amesema chupa za vinywaji zilizotoka kutumiwa na mtumiaji zinapotumika kama vifungashio huweza kupeleka mlaji kukumbana na athali mbali mbali za kiafya na kuomba wananchi kuepuka kununua hasa maziwa na mafuta ya kula ambayo yamefungwa katika chupa za maji na soda ambazo tayari zimekwisha kutumika.

Aidha Bw. Mosh amewasihi sana wajasiliamali na wafanyabiashara kuhakikisha wanafunga bidhaa zao za chakula na vinywaji katika vifungashio vinavyoruhusiwa na shirika la viwango Tbs ili kulinda afya ya mlaji.
Kwa upande wao baadhi ya wananchi wamesema mtindo wa maisha na uhaba wa elimu imekuwa ni moja ya chanzo kinachopelekea kutumia vitu vingi bila kujali usalama wa afyya zao.
Hata hivyo wananchi hao wameongeza kuwa serikali inawajibu wakuendelea kusimama kidete kuhakikisha wanaotumia makopo kufungashia bidhaa mbali mbali wanachukuliwa hatua za kisheria.