Joy FM
Joy FM
8 April 2026, 13:02

Mradi unagharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.9 ambapo utakapokamilika utawarahisishia wananchi kupata huduma sambamba na kuimarisha utendaji kazi kwa watendaji kutokana na matumizi ya jengo hilo.
Na Kadislaus Ezekiel
Wananchi katika Halmashauri ya wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, wamepongeza serikali kwa kutenga fedha kiasi cha zaidi ya bilioni mbili, ili kujenga ofisi za kisasa za Halmashauri hiyo, ikiwa ni mkakati wa kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi katika eneo moja, na kuondoa usumbufu kwa jamii kutembea umbali mrefu kusaka huduma.
Ujenzi wa mradi wa ofisi za Halmashauri hii ya Kibondo, unaendeela kufikia hatua za mwishoni, matumaini makubwa yakija kwa wananchi kurahisisha upatikanaji wa huduma katika eneo moja, na kuokoa mda wa kutafuta ofisi za idara tofauti.

Katika taarifa ya kaimu mhandisi mkuu wa idara ya miundombinu Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo Edwin Edward, amesema mradi huo upo katika hatua za mwishoni, na shughuli zilizobaki zinaendelea kufanyiwa kazi kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.