Joy FM

Nini suluhisho la rushwa ya ngono kwa wanawake?

1 April 2026, 15:17

Wanawake wafanyabiashara ya mazao ya uvuvi wakiendelea na shughuli ya uchuuzi wa samaki mwalo wa Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji, Picha na Tryphone Odace

Wanawake wafanyabiashara wengi wao wanasisitiza uwepo wa mazingira ya haki na heshima ili waweze kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya uchumi wa mkoa na taifa kwa ujumla.

Na Orida Sayon na Tryphone Odace

Wanawake wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi Mkoani Kigoma wamelalamikia kuendelea kukumbana na vitendo vya rushwa ya ngono, hali wanayosema inarudisha nyuma jitihada zao za kujikwamua kiuchumi na kufikia usawa wa kijinsia.

Simulizi ya Makala inayohusu madhira ya rushwa ya ngono kwa wanawake wafanyabiashara ya mazao ya uvuvi ziwa Tanganyika Mkoani Kigoma