Joy FM

Kibondo yaboresha barabara za mitaani kwa kiwango cha lami

27 March 2026, 11:12

Meneja wa TARURA Wilaya ya Kibodo Mhandisi Dickson Kanyankole, akiwa na viongozi wengine wakiwa wametembelea barabara inajengwa, Picha na Tryphone Odace

Wananchi Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wameiomba serikali kupitia TARURA kuboresha barabara zote za mitaani ili ziweze kupitika kwa urahisi ili ziweze kuchochea maendeleo kupitia shughuli za usafirishaji

Na Mwandishi wetu

Seikali imeanza kuchukua hatu za kujenga barabara za mitaani kwa kiwango cha lami nzito katika Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma, hatua inayolenga kupunguza changamoto ya miundombinu ya barabara pamoja na tope pamoja na vumbi, ambapo wananchi wameomba mkandarasi kusimamiwa ili mradi ukamilike kwa wakati.

Mafundi wakiendelea na ujenzi wa karavati katia barabara inajengwa Kibondo, Picha na Tryphone Odace

Wilaya ya Kibondo ina asili ya udongo mwekundu, ambapo kwa wageni, nyakati za masika hukutana na tope la kutosha, huku kiangazi ukikutana na vumbi kero zilizowatesa wananchi kwa kipindi kirefu, kilio ambacho kimeanza kutatuliwa mara baada ya kuanza ujenzi wa barabara za mitaani kwa kiwango cha lami, ikiwa ni hatua kubwa ya maendelea na wananchi wakitoa shime kwa serikali kwa kuanza ujenzi wa barabara hizo.

Sauti ya wananchi Kibondo

Katika hatua nyingine wananchi wameomba barabara za kuingia stendi ya mabasi kufanyiwa kazi pia ili njia hizo zipitike bila shida, kwani mabasi yamekuwa yakikwama mara kwa mara kutokana na wingi wa tope nyakati za masika.

Muonekano wa barabara inayojengwa kwa kiwango cha lami wilaya Kibondo, Picha na Tryphone Odace

Meneja wa wakala wa barabara za vijijini na mijini TARURA Wilaya ya Kibodo Mhandisi Dickson Kanyankole, amesema wanaendela kuchukua hatua za kuongeza mtandao wa barabara za lami, ili kuhakikisha hadhi ya mji wa kibondo unakuwa kwa kasi.

Sauti ya Meneja wa TARURA Wilaya ya Kibodo Mhandisi Dickson Kanyankole