Joy FM

Waoteshaji miti wataka elimu ya upandaji miti itolewe Kibondo

16 March 2026, 12:11

Muonekano wa miche ya miti ikiwe kwenye kitalu kabla ya kupelekwa sambani kupandwa, Picha na Mwandishi wetu

Utunzaji wa mazingira ni jambo muhimu kwa maisha ya binadamu na viumbe wengine duniani na katika miaka ya hivi karibuni, dunia imekumbwa na changamoto kubwa ya mabadiliko ya tabianchi ambayo imesababisha mabadiliko ya hali ya hewa kama vile ukame, mafuriko na ongezeko la joto duniani.

Na Mwandishi wetu

Baadhi ya waoteshaji wa miti ya kutunza mazingira Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wameiomba serikali kuendelea kutoa elimu ya upandaji wa miti  itakayosaidia katika kutunza mazingira na kupunguza hewa ukaa.

Hayo yameelezwa na Bw. Eliakimu Bitabo pamoja na Bi. Seili Eliakimu wakati wakiongea na Redio Joy Fm  kwenye bonde la  kijiji cha Kumwambu kata ya Kumwambu

Wamesema upandaji wa miti husaidia kuzuia ongezekola hewa ukaa na kuongeza kinga dhidi ya mafuriko na mmomonyoko wa udongo hasa maeneo yenye mwinuko.

Sauti ya Eliakimu Bitabo pamoja na Bi. Seili Eliakimu waoteshaji miti

Hata hivyo mpango wa halmashauri ya wilaya ya Kibondo ni kupanda miti milioni 1 na laki 5 kila mwaka kutoka kwenye vitalu vya wakala wa huduma za misitu TFS ambao wamekuwa wakiwagawia wananchi miti ya kupanda kwenye maeneo yao.