Joy FM

Viongozi wa dini waaswa kuhubiri amani, upendo na mshikamano Kasulu

11 March 2026, 12:53

Washiriki wa iftar katika wilaya ya Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Mkuu wa Wilaya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu amesema katika kipindi hiki cha mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani na Kwaresma kwa wakristo viongozi wa dini hawana budi kuendelea kuwaunganisha waumini wao ili kuweza kuishi kwa upendo

Na Hagai Ruyagila

Viongozi wa dini wilayani Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kuendelea kuhubiri amani, upendo na mshikamano kwa waumini wao ili kudumisha hali ya utulivu na umoja katika jamii.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu wakati akizungumza katika hafla ya iftari iliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kushirikiana na shirika la Posta Tanzania ikiwakutanisha viongozi mbalimbali wa dini wilayani humo.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu katika iftar iliyoandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu pamoja na Posta Tanzania, Picha na Hagai Ruyagila

Kanali mwakisu Amesema viongozi wa dini wana nafasi kubwa katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kudumisha amani na kuepuka vitendo vinavyoweza kuleta migogoro au kuvuruga utulivu wa nchi.

Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu

Mwenyekiti wa BAKWATA wilaya ya Kasulu Shekhe Ruhettah Ahmad Hussein amesema mwezi mtukufu wa Ramadhani ni fursa muhimu kwa waumini kuimarisha ibada, kusaidiana na kudumisha amani, huku akiwataka waumini kuwa na umoja katika jamii.

Mwenyekiti wa BAKWATA wilaya ya Kasulu Shekhe Ruhettah Ahmad Hussein Picha na Hagai Ruyagila

Sauti ya Mwenyekiti wa BAKWATA wilaya ya Kasulu