Joy FM

Madiwani watakiwa kufanya kazi kwa uwazi na weledi Kigoma

5 March 2026, 09:05

Baadhi ya madiwa wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa katika mafunzo, Picha na Ofisi ya mawasiliano Kigoma Ujiji

Kuwajengea uwezo madiwani kunachangia uongozi bora, uwajibikaji, na utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo, jambo ambalo linaongeza ustawi wa wananchi katika ngazi ya kata na Halmashauri.

Na Mwandishi wetu

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Sospeter Mtwale amewataka madiwani Nchini kote kusimamia Halmashauri kwa uwazi, weledi na ufanisi katika kuleta Maendeleo ya Wananchi.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Sospeter Mtwale akiwa katika mkutano wa kuwajengea uwezo madiwani Manispaa ya Kigoma Ujiji, Picha na Ofisi ya mawasiliano Kigoma Ujiji

Ameyasema hayo alipokuwa akifunga mafunzo elekezi kwa madiwani Kitaifa yaliyofanyikia Manispaa ya Kigoma Ujiji Mkoani Kigoma.

Amewataka madiwani kwa kushirikiana na wataalamu katika kutatua migogoro ya wananchi, kukuza mapato na kusimamia miradi ya maendeleo kwa fedha kutoka Serikali Kuu na mapato ya ndani.

Baadhi ya madiwa wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wakiwa katika mafunzo, Picha na Ofisi ya mawasiliano Kigoma Ujiji

Aidha amewataka kuwa waadilifu na kutanguliza maslahi ya Wananchi katika Utekelezaji wa Majukumu yao.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) Sospeter Mtwale, Picha na Ofisi ya Mawasiliano ya Manispaa ya Kigoma Ujiji

Katibu Tawala wa Wilaya Mganwa Nzota akitoa salamu za Mkoa kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa amewataka kuzingatia mafunzo waliyoyapata katika kusimamia Halmashauri kwa kukuza Mapato, utekelezaji wa miradi na kutatua migogoro ya Wananchi.

Katibu Tawala wa Wilaya Ndugu. Mganwa Nzota akizungumza katika kikao hicho, Picha na Ofisi ya mawasiliano Manispaa ya Kigoma Ujiji

Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mhe. Mussa Maulidi amekipongeza Chuo cha Serikali za Mitaa kwa namna ambavyo kimetoa mafunzo kwa Halmashauri 184 Nchi kote huku akisema wataendelea kusimamia kwa kuzingatia kanuni, taratibu na sheria.

Meya wa Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mhe. Mussa Maulidi, Picha na Ofisi ya mawasiliano Manispaa ya Kigoma Ujiji