Joy FM
Joy FM
13 February 2026, 14:15

Halmashauri ya Mji wa Kasulu Mkoani Kigoma imewataka walimu wakuu wa shule za Sekondari kuhakikisha wanasimamia nidhamu ili kuongeza ufaulu
Na Hagai Ruyagila
Wakuu wa Shule za Sekondari katika Halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kusimamia suala la nidhamu kwa waalimu na wanafunzi ili kuhakikisha wanaongeza ufaulu kwa wanafunzi.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mji Kasulu mwl Vumilia Simbeye wakati Akifungua kikao cha awali cha umoja wa wakuu wa Shule TAHOSSA chenye lengo la kujadili masuala mbalimbali ikiwemo suala la taaluma na nidhamu shuleni.
Mwl Simbeye amesisitiza kusimamia ipasavyo mienendo ya nidhamu kwa waalimu na wanafunzi Pamoja na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

Aidha ameongeza kwa kuwataka wakuu wa shule kushirikiana na wazazi kudhibiti suala la utoro pamoja na kukemea tabiaa za baadhi ya waalimu wanaofanya shughuli binafsi muda wa vipindi darasani.
Akizungumza kwa niaba ya wakuu wa shule ambao wameshiriki kikao hicho, Mkuu wa shule ya Sekondari Kigoma Gland Mwl Severino manyota wamehiadi kutekeleza na kusimamia maagizo hayo.

Baadhi ya wananchi wameeleza matarajio na manufaa yao ikiwa waalimu hao watasimamia nidhamu shuleni pamoja na kudhibiti suala la utoro kwa waalimu na wanafunzi.