Joy FM

Kigoma watakiwa kuchangamkia fursa zitokanazo na taka

30 January 2026, 18:15

Muonekano wa takataka mchanganyiko ambazo zinafanyiwa urejeshi kutajwa husaidia kuinua uchumi wa wananchi, Picha na Lucas Hoha

Taka kwa muda mrefu zimekuwa zikichukuliwa kama vitu visivyo na maana na vinavyosababisha uchafuzi wa mazingira, hata hivyo kwa sasa dunia imeanza kubadilisha mtazamo huo kwa kuona taka kama rasilimali muhimu inayoweza kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Na Lucas Hoha

Wanachi Mkoani wa Kigoma wametakiwa kuchangamkia fursa za kiuchumi zinatokana na taka za plastiki, vyuma chakavu na taka za mabaki yatokanayo na zao la mchikichi ili kuinua hali zao kimaisha.

Muonekano wa takataka mchanganyiko ambazo zinafanyiwa urejeshi kutajwa husaidia kuinua uchumi wa wananchi, Picha na Lucas Hoha

Hayo yamebainishwa na baadhi ya wafanyabiashara wanaotumia fursa za vyuma chakavu na taka za plastiki kwa kuzikusanya taka na kuziuza viwandani  kwa kuwezeshwa na shirika la Catholic Relief Service (CRS) wakishirikiana na Shirika la Caritas chini ya ufadhili wa Umoja wa Ulaya kupitia mradi wa usimamizi wa taka na usafi wa mazingira (VOICES).

Baadhi ya wafanyabiashra hao akiwemo Idrisa Musa ambaye anakusanya vyuma  chakavu katika Kata ya Mwandiga Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wanaeleza namna kazi hiyo ya uchumi rejeshi inavyowasaidia kuondokana na umasikini.

Sauti za baadhi ya wafanyabiashra wa vyuma chakavu Kigoma
Idrisa Musa ambaye anakusanya vyuma  chakavu katika Kata ya Mwandiga Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Picha na Lucas Hoha

Kwa upande wake, Hassan Kilanoza ambaye ni mmiliki wa kiwanda cha kukamua mafuta ya mawese katika kata ya Simbo anaeleza namna anavyotumia mabaki ya mchikichi baada ya kukamua mafuta kuzalisha mkaa mbadala na kujiingizia kipato.

Sauti ya Hassan Kilanoza ambaye ni mmiliki wa kiwanda cha kukamua mafuta ya mawese
Hassan Kilanoza ambaye ni mmiliki wa kiwanda cha kukamua mafuta ya mawese katika kata ya Simbo anatumia mabaki ya mchikichi kuzalisha mkaa mbadala, Picha na Lucas Hoha

Simon Mwanjela ni Afisa mradi Mwandamizi kutoka shirika la Catholic Relief Sevirce (CRS) lililopo Manispaa ya Kigoma Ujiji jengo la NSSF anasema vijana wenye mawazo ya ubunifu wa kutumia taka za plastiki kuwa fursa ya kujikwamua kiuchumi watawezeshwa mitaji.

Sauti ya Afisa mradi Mwandamizi kutoka shirika la Catholic Relief Sevirce (CRS)

Mradi huo umeanza kutekelezwa tangu mwaka 2024 na utafikia kikomo mwaka 2028 na unatekelezwa katika halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, Manispaa ya Kigoma Ujiji na Wilaya Kigoma, ukiwa na  lengo la kuwafikia watu zaidi ya laki moja.

Muonekano wa takataka mchanganyiko ambazo zinafanyiwa urejeshi kutajwa husaidia kuinua uchumi wa wananchi, Picha na Lucas Hoha