Joy FM

Madiwani watakiwa kusimamia miradi ya maendeleo Kasulu

28 January 2026, 12:53

Mkuu wa Mkoa Kigoma, Balozi Simon siro akizungumza  katika mkutano wa madiwani Halmashauri ya wilya ya Kasulu, Picha na Emmanuel Kamangu.

Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya Kasulu wametakiwa kuendelea kusimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao ili iweze kuwa na ubora unaokusudiwa

Na Emmanuel Kamangu

Mkuu wa Mkoa wa kigoma IGP Mstafu Balozi Simon Sirro amewataka madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu kuzingatia maadili ya utumishi pamoja kusimamia shuguli za maendeleo kikamilifu.

Balozi Sirro amebainisha hayo wakati akizungumza na madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ambapo amewataka kusimamia maendeleo ya wananchi kwa vitendo na kujitenga na rushwa ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za kijamii.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa kigoma IGP Mstafu Balozi Simon Sirro
Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wakiwa katika kikao cha baraza la madiwani, Picha na Emmanuel Kamangu.

Aidha Balozi siro amewataka madiwani kuhamasisha wananchi kujikita katka  kilimo cha biashara ili kuweza kujikwamua kiuchumi.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa kigoma IGP Mstafu Balozi Simon Sirro

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanal Isack Mwakisu amewaomba madiwani kutembea katika kile alichoelekeza balozi Siro hasa kwa kuendelea kuhakikisha  wanannchi wao  wanaendelea kupewa elimu ya   kufuga na kulima kisasa.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanal Isack Mwakisu, Picha na Emmanuel Kamangu
Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanal Isack Mwakisu

Baadhi ya madiwani katika Halmashauri hiyo wameahidi kufanyia kazi maelekezo ya mkuu wa mkoa Balozi siro  ili kuhakikisha wanawatumikia wananchi kwa uadirifu na kuwaletea maendeleo.

Sauti ya madiwani