Joy FM

Kigoma watakiwa kuzingatia lishe bora kwa watoto

31 December 2025, 12:38

Ukosefu wa lishe bora kwa watoto unatajwa kuwa chanzo cha kuongezeka kwa udumavu pamoja na ugonjwa wa utapiamlo jambo ambalo hupunguza uwezo wa kufanya vizuri shuleni pamoja na ufanisi katika maisha ya utu uzima.

Na Esperance Ramadhan

Katika kuendelea  kuhakikisha jamii inakuwa na afya njema, Jamii imetakiwa kutekeleza afua za lishe kwa kutoa elimu ya afya na lishe kwa wazazi na walezi.

 Lishe bora ni msingi mzuri wa afya bora na  inachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya  ukuaji wa kimwili na kiakili kwa mtoto.

Kwa kutambua ukubwa na umuhimu wa kuondokana na udumavu kwa watoto Afisa mtendaji wa mtaa wa rutale kata ya kipampa Bw Mathayo Edward amesema  tangu kuanzishwa kwa  siku ya afya na lishe ya kijiji (SALIKI) imesaidia kuwapa elimu  wazazi na walezi namna ya kuandaa lishe bora na kupunguza  hali ya udumavu wa watoto.

Sauti ya Afisa mtendaji wa mtaa wa rutale kata ya kipampa Bw Mathayo Edward

Aidha amewataka wazazi na walezi kujitokeza katika  siku ya afya na lishe ya kijiji  SALIKI ili kuendelea kupata elimu ya uandaaji mzuri wa  chakula cha watoto kwa  kuzingatia makundi sita ya chakula.

Sauti ya Afisa mtendaji wa mtaa wa rutale kata ya kipampa Bw Mathayo Edward

Kwa upande wao, Baadhi ya wazazi waliyopatiwa elimu wamesema wataitumia katika familia zao na kuhamasisha jamii inayowazunguka kwa kuwapa  elimu waliyoipata wao.

Sauti ya baadhi ya wazazi

Takwimu za 2023 zinaonyesha mkoa wa Kigoma ulifanya vizuri katika kupambana na utapiamlo ingawa changamoto ya kutokula mlo kamili bado ipo na inahitaji juhudi zaidi katika kuhamasisha lishe bora.