Joy FM

Wazazi, walezi waaswa kuwalinda watoto Kigoma

23 December 2025, 08:37

Waumini wa kanisa la EAGT Mwasenga wakiwa katika sherehe za watoto, Picha na Prisca Kizeba

Jukumu la msingi la wazazi na walezi ni kuhakikisha watoto wanalindwa, wanalelewa kwa upendo na wanaishi katika mazingira salama ili waweze kufikia ndoto zao na kuchangia maendeleo ya jamii.

Na Prisca Kizeba

Wazazi na walezi wanapotekeleza wajibu wao ipasavyo, jamii hunufaika kwa kuwa na vijana wenye nidhamu na kuepuka ongezeko la uhalifu na vitendo viovu.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa kituo cha Compassion Mwasenga Robart Petro  wakati wa ugawaji wa zawadi za krismasi kwa watoto na wazazi wenye hali ya chini , nakuwaasa wazazi kuwa makini katika uangalizi wa watoto wao.

Sauti ya Mkurugenzi wa kituo cha Compassion mwasenga Robart Petro

 Sambamba na hayo, Mkurugenzi amewaomba wazazi  kuwatia moyo na kuendeleza vipaji vya watoto  na kuacha tabii ya kuwavuja moyo pale mtoto anapoonyesha kipaji chake.

Sauti ya Sauti ya Mkurugenzi wa kituo cha Compassion mwasenga Robart Petro

 Akitoa ufafanuzi wa zawadi hizo, Mhasibu wa Maleni Josephu na kusema kwa wametoa zawadi zenye dhamani ya shilingi milioni sita laki nane na elfu stina na tisa na mia saba.

Sauti ya Mhasibu wa Maleni Josephu

Baadhi ya wazazi wametoa shukrani zao na hapa wanaeleza furaha yao baada ya kupokea zawadi hizo.

Sauti ya Wananchi Mwasenga