Joy FM

Watoto yatima wakumbukwa Kigoma

22 December 2025, 09:47

Watoto wanaolelewa katika kituo cha Subira minal rahman wakiwa kwenye picha na uongozi wa Lupimo Sanitarian Clinic walipotembelea kituo hicho na kutoa misaada, Picha na Tryphone Odace

Jamii na wadau mbalimbali mkoani Kigoma wameaswa kujitokeza na kuwasaidia watoto yatima na wenye uhitaji ili nao waweze kujiona wanathaminiwa na jamii inayowazunguka.

Na Tresiphol Odace

Kituo cha tiba mbadala cha Lupimo Sanitarian Clinic kimetoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto yatima yanaolelewa katika kituo cha Subira Minal rahman kilichopo Kitongoni Manispaa ya Kigoma Ujiji ikiwa ni sehemu ya kituo hicho kurudisha fadhila kwa jamii.

Meneja Mkuu wa Lupimo Sanitarian Clinic Dkt. Emmanuel Madila amesema lengo la kutoa msaada huo ni kutaka kuoana watoto hao ambao wengi wao hawana baba wala mama wanajiona wakithaminiwa kama watu wengine huku akipongeza uongozi wa kituo hicho kwa namna ambavyo wameendelea kuwalea watoto na kuwapa madili mazuri.

Sauti ya Meneja Mkuu wa Lupimo Sanitarian Clinic Dkt. Emmanuel Madila
Vitu mbalimbali vilivyotolewa kwa watoto yatima wa kituo cha kulea watoto cha Subira Minal rahman, Picha na Tryphone Odace

Awali Mwenyekiti wa Kituo cha Subira Minal Rahaman Bi. Khadija Mpezi amekipongeza kituo cha Lupimo kwa msaada huo na kuwaomba wadau wengine kuendelea kuwasaidia watoto huku Ust Abel Mukoko ambaye ni ustadhi wa madrasa ya Subira Minal Rahan akieleza namna wanavyohudumia watoto hao.

Sauti ya Mwenyekiti wa Kituo cha Subira Minal Rahaman Bi. Khadija Mpezi

Hata hivyo, Kaimu Meneja wa Lupimo Sanitarian Clinic Aston Ngao amesema wametembelea kituo hicho na kuwapa msaada huo wa chakula siku ya sikuku za krismas na mwaka mpya.

Sauti ya Kaimu Meneja wa Lupimo Sanitarian Clinic Aston Ngao
Watoto wanaolelewa katika kituo cha Subira minal rahman wakiwa kwenye picha na uongozi wa Lupimo Sanitarian Clinic walipotembelea kituo hicho na kutoa misaada, Picha na Tryphone Odace

Kituo cha Subira Minal Rahaman kinalea jumla ya watoto yatima na wanaoishikatika mazingira magumu 145 na vituo vilivyotolewa na kituo cha Lupimo Sanitarian Clinic ni pamoja na vyakula, mafuta, mikeka na vinywaji vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi laki saba na pesa taslim zaidi ya shilingi laki mbili.