Joy FM

Bilioni 1 kupatikana kupitia soko la mwanga Kigoma

19 December 2025, 14:09

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Kisena Mabuba akiwa anapata maelezo kutoka kwa mkandarasi anayekeleza ujenzi wa soko la mwanga, Picha na Lucas Hoha

Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo inatajwa kuchochea uchumi na kipato kupitia mapato yatokanayo na miradi hiyo

Na Lucas Hoha

Manispaa ya Kigoma Ujiji inatarajia kukusanya zaidi ya shilingi bilioni 1 kwa mwaka kutoka chanzo cha mapato cha soko la mwanga linaloendelea kujengwa tofauti na awali ambapo Manispaa ilikuwa ikikusanya shilingi  milioni 4 kwa mwaka

Akizungumza na waandishi wa habari wakati mara baada ya kutembelea miradi  inayotekelezwa na Serikali, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Kisena Mabuba amesema serikali imedhamiria kufungua Mkoa wa Kigoma kiuchumi kwa kutekeleza miradi ya kimkakati.

Amesema kutokana na uwepo wa soko la Mwanga na miradi mingine itasaidia manispaa kujiendesha kutokana na ukusanyaji wa mapato.

Sauti ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Kisena Mabuba
Muonekano wa mradi wa ujenzi wa soko la Mwanga Manispaa ya Kigoma Ujiji, Picha na Lucas Hoha

Aidha ameongeza wakati soko hilo linavunjwa wapo wafanyabiashara waliohamishwa hivyo ujenzi wa soko utakapokamilika watapewa kipaumbele wale ambao walikuwepo awali ili kuondoa migogoro.

Akizungumzia soko hilo, Mkandarasi mjenzi wa soko la Mwanga amesema ujenzi wa soko hilo umefikia asilimia 43 nakuwa wamechelewa kukamilisha mradi huo kutokana na mvua zilizonyesha mfululizo nakuwa ifikapo mapema mwaka 2026 wanakamilisha mradi huo.

Sauti ya Mkandarasi mjenzi wa soko la Mwanga