Joy FM

Jamii yaaswa kuwalinda watoto dhidi ya ukatili

8 December 2025, 16:23

Baadhi ya watumishi wa mungu waliotembelea na kutoa msaada katika gereza la Bangwe, Picha na Prisca Kizeba

Wito umetolewa kwa jamii kuendelea kukemea vitendo vya ukatilii ambavyo vimekuwa vikifanyika kwa jamii

Na Prisca Kizeba

Wanawake Katika Manispaa ya Kigoma Ujiji wameaswa kuwalinda watoto wao dhidi ya vitendo vya ukatili unaoendela katika jamii

Hayo yamesemwa na Afisa Ustawi wa jamii Exavery Nkyami wakati wa maombi  kumshukuru Mungu kwa kumaliza mwaka salama  kwa wanawake  wa kanisala TAG     ambapo amesema kila mwanamke anawajibu wa kulinda mtoto wake ili kuhakikisha mtoto hafanyiwi ukatili

 Naye Mwangalizi wa section hiyo Dkt. Galishoni amesema wanawake wanao wajibu wa kutunza ndoa zao ili kuwa na utumishi bora katika jamii na kanisa kwa ujumla

 Sambamba na hayo,  Wanawake hao wamehitimisha kwa kutembelea wafungwa katika gereza la Bngwe na kutoa zawadi mbalimbali kwa wafungwa wa gereza la Bangwe.

Maaskari wa gereza la bangwe wakipokea msaada uliotolewa na watumishi wa mungu, Picha na Prisca Kizeba

Akipokea zawadi  hizo Mkaguzi Msaidizi wa magereza afande Arnold ametoa shukrani na kuwaasa kuendelea kuwa na moyo huohuo ili kuwa mabalozi kwa watu wengine

Nayea mwenyekiti wawanawake Liliani Magesa amesema kuwa kila mtu anao wajibu wakujitoa kuwasadia watu wengine waliopo kwenye matazizo ili kuwa na utumishi ulio kamilika

Baadhi ya wanawake waliohudhuria maombi hayo wamekuwa na haya yakueleza kuhusu ukatili