Joy FM

Vyombo vya ukamataji na upelelezi vyaaswa kufanya kazi kwa weledi

8 December 2025, 09:06

Watumishi kutoka taasisi za ukamataji na upelelezi wakiwa kwenye mafunzo, Picha na Hagai Ruyagila

Vyombo vya ukamataji na upelelezi mkoani Kigoma, vimetakiwa kutotumia vibaya madaraka badala yake vifuate kanuni za ukamataji na kuhakikisha kwamba suala la upelelezi na uchunguzi wa mashauri linafanyika kwa uadilifu weledi na uwajibikaji wa hali ya juu ili kuepuka kuharibu kesi, kusababisha kero kwa watu kwa kutotenda haki.

Na Hagai Ruyagila

Watumishi wa taasisi za NPS, TAKUKURU, Jeshi la Polisi na Uhamiaji Mkoani Kigoma wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na kufuata sheria ili kuhakikisha wananchi wanapata haki zao kwa wakati na kuzingatia huduma bora za mashitaka na usawa kwa wote.

Hayo yamejiri wakati wa kuhitimisha mafunzo ya Siku mbili ambayo yamezikutanisha taasisi za watumishi wa NPS,TAKUKURU,jeshi la Polisi na idara ya uhamiaji mafunzo ambayo yamefanyika mjini Kasulu ambapo mada 9 zimetolewa kwa Watumishi hao.

Mkuu wa mashitaka Mkoa Wa Kigoma Waziri Magumbo Anaeleza dhima ya mafunzo hayo katika kuhakikisha wanapunguza mrundikano wa mashauri Mahakamani.

Sauti ya Mkuu wa mashitaka Mkoa Wa Kigoma Waziri Magumbo

Kwa upande wake, Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kigoma Alfred Kasoro amewataka watumishi hao kuyatumia mafunzo waliyopatiwa kuleta ufanisi kwa wananchi kwa kutenda haki.

Sauti ya Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kigoma Alfred Kasoro

Afisa uhamiaji Mkoa wa Kigoma kamishina msaidizi mwandamizi Dismas Mulura amehimiza kufanya kazi kwa ushirikiano.

Sauti ya Afisa uhamiaji Mkoa wa Kigoma kamishina msaidizi mwandamizi Dismas Mulura

Akifunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya Ya Kasulu Kanali Isaac Mwakisu, Katibu tawala wilaya ya Kasulu Bi.Theresia Mtewele ametoa wito wa kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

Sauti ya Katibu tawala wilaya ya Kasulu Bi.Theresia mtewele
Katibu tawala wilaya ya Kasulu Bi.Theresia Mtewele, Picha na Hagai Ruyagila