Joy FM

Vyombo vya ukamataji na upelelezi vyatakiwa kufuata kanuni za ukamataji

5 December 2025, 13:44

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma Augustino Rwizile akiwa na viongozi wengine wakiwa kwenye semina, Picha na Emmanuel Matinde

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania amehimiza watendaji wa vyombo vinavyohusika na ukamataji na upelelezi kufuata taratibu na sheria

Na Emmanuel Matinde

Vyombo vya ukamataji na upelelezi mkoani Kigoma, vimetakiwa kutotumia vibaya madaraka badala yake vifuate kanuni za ukamataji na kuhakikisha kwamba suala la upelelezi na uchunguzi wa mashauri linafanyika kwa uadilifu weledi na uwajibikaji wa hali ya juu ili kuepuka kuharibu kesi, kusababisha kero kwa watu kwa kutotenda haki.

Kauli hiyo imetolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma,  Augustino Rwizile, wakati akifungua mafunzo ya weledi kwa wapelelezi na waendesha mashtaka wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka NPS Mkoa wa Kigoma, yaliyojumuisha pia TAKUKURU na Uhamiaji.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma Augustino Rwizile akiwa na viongozi wengine wakiwa kwenye semina, Picha na Emmanuel Matinde

Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Ofisi za Halmashauri ya Mji Kasulu, yakilenga kujengeana uwezo wa upelelezi wa makosa ya jinai na kuendesha mashtaka, kubadilishana uzoefu wa kiutendaji katika masuala ya upelelezi pamoja na uendeshaji wa mashtaka.

Sauti ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Kigoma

Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kigoma Alfred Kasoro, na Mkuu wa Mashtaka Mkoa wa Kigoma Waziri Magumbo, wameeleza katika mafunzo hayo namna wanavyoumizwa na suala la baadhi ya wapelelezi na wachunguzi kukosa weledi na kusababisha kukwama mahakamani.

Sauti ya Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kigoma Alfred Kasoro, na Mkuu wa Mashtaka Mkoa wa Kigoma Waziri Magumbo

Awali Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU Mkoa wa Kigoma, Asha Kwariko, amesema kwa pamoja wamejipanga kuhakikisha mlolongo wa haki jinai unatekelezwa kwa ufanisi katika mkoa wa Kigoma.

Sauti ya Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini TAKUKURU Mkoa wa Kigoma, Asha Kwariko