Joy FM

Nyavu haramu 197 zateketezwa Uvinza

5 December 2025, 09:05

Muonekano wa nyavu haramu ambazo zimeteketezwa na Serikali ya Wilaya Uvinza, Picha na Ofisi ya Mawasiliano Uvinza

Mkuu wa Wilaya Uvinza Mkoani Kigoma Dinah Mathamani amesema wataendelea kufanya oparesheni ili kubaini na kukamata nyavu haramu zinazotumiwa na wavuvi ndani ya ziwa Tanganyika

Na Mwandishi wetu

Serikali wilayani Uvinza imeziteketeza nyavu haramu 197 katika Kijiji cha Rubengela kata ya Sunuka Leo tarehe 4 Desemba,2025 ikiwa ni sehemu ya juhudi za kudhibiti uvuvi haramu katika Ziwa Tanganyika.

Muonekano wa nyavu haramu zilizokamatwa na kuteketezwa na Serikali Wilayani Uvinza, Picha na Ofisi ya mawasiliano Uvinza

Zoezi hilo limefanyika chini ya usimamizi wa Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mh. Dinah Mathamani, ambaye aliongoza viongozi na maafisa uvuvi katika kuhakikisha nyavu hizo hazirejei tena kwenye matumizi.

Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mh. Dinah Mathamani na viongozi wengine, Picha na Ofisi ya Mawasiliano Uvinza

Mh. Mathamani amesisitiza kuwa serikali haitavumilia mtu yoyote anayejihusisha na uvuvi haramu, kwa kuwa vitendo hivyo vinaharibu mazalia ya samaki na kuhatarisha uchumi wa wavuvi wanaofuata sheria. Ameeleza kuwa oparesheni za kukamata na kuteketeza zana haramu ni endelevu na zitafanyika katika maeneo yote ya Wilaya Uvinza.

Aidha, wananchi wa Rubengela wamepongeza serikali kwa kuchukua hatua hiyo, wakisema kuwa uvuvi haramu umekuwa ukipunguza sana upatikanaji wa samaki na kuathiri mapato ya kaya.

Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Mh. Dinah Mathamani na viongozi wengine, Picha na Ofisi ya Mawasiliano Uvinza