Joy FM

Ndalichako atoa gari la wagonjwa kituo cha afya Mwamintare Kasulu

4 December 2025, 12:13

Gari lililotolewa na Mbunge wa Kasulu Mjini Profesa Joyce Ndalichako, Picha na Hagai Ruyagila

Kituo cha afya cha Mwamintare kilichopo Halmashauri ya Mji wa Kasulu kinahudumia kata tatu ya Muhunga, Mganza na Heru Juu kwa wakazi 50887.

Na Hagai Ruyagila

Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini mkoani Kigoma Profesa Joyce Ndalichako amekabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha Afya cha Mwamintare kilichopo kata ya Heru Juu Halmashauri ya Mji Kasulu ili kuwasaidia kuimarisha utoaji wa huduma za dharura kwa wananchi wa eneo hilo.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano Profesa Ndalichako amesema kukabidhi gari hilo ni sehemu ya jitihada ya kuboresha sekta ya afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa haraka na usalama wanapopata dharura.

Sauti ya Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini mkoani Kigoma Profesa Joyce Ndalichako
Mbunge wa Kasulu Mjini Profesa Joyce Ndalichako akisalimiana wakati wa kukabidhi gari la wagonjwa, Picha na Hagai Ruyagila

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye ameishukuru serikali kupitia mbunge huyo kwa msaada huo akibainisha kuwa gari hilo litapunguza changamoto ya usafiri wa wagonjwa na kuongeza ufanisi wa huduma bora za afya katika eneo hilo.

Sauti ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Kasulu Mwl. Vumilia Simbeye

Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Kasulu Mh. Ayubu Ngalaba, amewataka watumishi wa kituo gicho pamoja na wananchi kulitunza gari hilo na kuhakikisha linatumika kwa kazi iliyokusudiwa ili liendelee kutoa manufaa kwa muda mrefu.

Sauti ya Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji Kasulu Mh. Ayubu Ngalaba

Awali, akisoma taarifa ya kituo hicho, Mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Mwamintare Dr. Mgoba John amesema upatikanaji wa gari hilo utasaidia kusafirisha wagonjwa kwa haraka hali ambayo itasaidia kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na vifo vya watoto.

Sauti ya Mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Mwamintare Dr. Mgoba John