Joy FM

Madiwani watakiwa kutumikia wananchi kwa uaminifu Kigoma

2 December 2025, 11:52

Madiwani wa Manispaa ya Kigoma Ujiji wakila kiapo cha uadilifu kwa utumishi wa umma, Picha na Mwandishi wetu

Madiwani katika Manispaa ya Kigoma Ujiji Mkaoni Kigoma wametakiwa kuhakikisha wanafuatilia na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi katika maeneo yao

Na Mwandishi wetu

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Elisante Mbwilo amewataka waheshimiwa madiwani kuwatumikia wananchi kwa uaminifu na uadilifu kama walivyoapa kwenye kiapo chao

Ameyasema hayo leo Desemba 02, 2025 alipokuwa akihutubia Mkutano wa kwanza wa baraza la madiwani Manispaa ya Kigoma Ujiji uliofanyika katika ukumbi wa NNSF Kigoma mara baada ya badiwani wateule kula kiapo cha utii na ahadi ya uadilifu kwa Viongozi wa Umma.

Kaimu Katibu tawala Mkoa wa Kigoma Elisante Mbwilo akihutubia baraza la madiwani manispaa ya Kigoma Ujiji, Picha na Mwandishi wetu

Aidha amewataka kusimamia vyema miradi ya maendeleo sambamba na ukusanyaji wa mapato kikamilifu na kuhakikisha Wananchi wanapata maendeleo.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Kisena Mabuba, Picha na mwandiahi wetu