Joy FM

Wazazi watakiwa kuchangia chakula shuleni Kibondo

24 November 2025, 12:32

Wananchi wa Kitahana Wilayani Kibondo wakiwa katika maadhimisho ya siku ya lishe, Picha na Dotto Josesphati

Wazazi na Walezi Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wametakiwa kuwa na desturi ya kuanda lishe bora kwa watoto

Na Dotto Josephati

Wazazi Wilayani Kibondo Mkoani Kigoma wanatakiwa kuongeza juhudi kwa kuwachangia chakula cha watoto wao shuleni ili iwasaidie kuongeza ufanisi wa kujifunza wanapokuwa katika masomo yao.

Wananchi wa Kata ya Kitahana wakiwa katika siku ya Lishe Kibondo, Picha na Dotto Josephati

Wito huo umetolewa na Afisa Mtendaji wa kata ya Kitahana Bw. Fundi Hamisi katika Kijiji cha Rugunga Kata ya Kitahana katika kilelecha maadhimisho ya siku ya lishe ambapo amesema upatikanaji wa chakula kwa watoto shuleni utawasaidia kujifunza katika mazingira mazuri pindi wanapokua shuleni.

Sauti ya Afisa Mtendaji wa kata ya Kitahana Bw. Fundi Hamisi

Naye afisa elimu Kata Bi. Zuwena Yusufu amesema watoto wanapopata chakula shuleni inawaidia kufanya vizuri katika masomo huku Afisa kilimo Bw. Rajabu  Ridhiwa akiwahimiza wananchi kujenga tabia ya kulima mbogamboga na matunda  angalau eneo dogo majumbani mwao ili iwasaidie kuboresha afya zao.

Sauti ya afisa elimu Kata Bi. Zuwena Yusufu

Kwa upande wake, Afisa lishe Wilaya ya Kibondo Bi. Jakline Sospita amewataka wazazi kuzingatia mlo kamili wanapokuwa wanaandaa chakula cha watoto wao ili wakue katika hali njema.

Sauti ya Afisa lishe Wilaya ya Kibondo Bi. Jakline Sospita