Joy FM

Viongozi watakiwa kuwatumikia wananchi Kasulu

20 November 2025, 11:32

Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika Mhashamu Emmanuel Bwatta, Picha na Hagai Ruyagila

Viongozi wametakiwa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu na uwajibikaji

Na Hagai Ruyagila

Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika Mhashamu Emmanuel Bwatta amewahimiza viongozi wa Dini na watumishi wa umma nchini kuwatumikia wananchi kwa nidhamu, uadilifu, uwazi na uwajibikaji ili kuendeleza misingi bora ya kuaminika katika jamii.

Akizungumza na waumini wa kanisa la Anglikana Kanda ya Kasulu Mjini, Askofu Bwatta amesema utumishi mzuri ni kiongozi kutumia nafasi yake kwa nidhamu na uadilifu vitu ambavyo ni nguzo muhimu katika kujenga utumishi bora unaoaminika, nakuwa manufaa kwa jamii anayoiongoza.

Sauti ya Askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Western Tanganyika Mhashamu Emmanuel Bwatta

Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana Kanda ya Kasulu Mjini, Canon James Bigombo amewasihi waumini wa dini ya Kikristo kuendelea kuliombea taifa ili amani iendelee kutamalaki.

Sauti ya Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana Kanda ya Kasulu Mjini, Canon James Bigombo
Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana Kanda ya Kasulu Mjini, Canon James Bigombo, Picha na Hagai Ruyagila

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana Kanda ya Manyovu, Canon Yohana Nyoka amewahimiza waumini wa dini ya Kikristo kumtumikia Mungu kwa uaminifu katika maisha yao.

Suti ya Mkurugenzi wa Kanisa la Anglikana Kanda ya Manyovu, Canon Yohana Nyoka

Baadhi ya waumini wa dini ya Kikristo wamesisitiza umuhimu wa viongozi wote kuwa na maadili na moyo wa utumishi.

Sauti ya waumini wa dini ya Kikristo