Joy FM

Mabalozi kutembelea kambi za wakimbizi Kigoma

18 November 2025, 11:50

Mkuu wa Mkoa Kigoma akiwa kwenye picha na Mabalozi wawakilishi wa nchi na wadau wa maendeleo, Picha Ofisi ya mawasiliano Kigoma

Serikali ya Mkoa wa Kigoma imewatoa shukrani kwa wawakilishi wa nchi na wadau wa maendeleo kwa kufanikisha kuendelea kufadhili miradi mbalimbali ya kijamii katika kambi za wakimbizi zilizopo Kigoma

Na Mwandishi wetu

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amekutana na mabalozi na wawakilishi kutoka kwenye balozi za nchi wadau wa Maendeleo, ambao wamewasili mkoani hapa leo Novemba 18, 2025 kwa ajili ya kutembelea Kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu wilayani Kasulu na Nduta wilayani Kibondo ili kujionea Shughuli zinazofanywa na Mashirika mbalimbali ya kuhudumia wakimbizi mkoani hapa.

Mkuu wa Mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro akiwa katika mazungumzo na wawakilishi wa nchi wadau wa maendeleo

Kupita Mazungumzo yao, Balozi Sirro ameyashukuru mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayohudumia wakimbizi kutoka nchini Burundi na Congo DR, yaliyopo katika Mkoa wa Kigoma sambamba na uwezeshaji wa shughuli mbalimbali za kijamii kwa wakazi wanaokaa katika maeneo yanayozunguuka kambi hizo unaoratibiwa na kutekelezwa na Program ya Pamoja ya Kigoma (KJP).

Aidha, ameueleza ujumbe huo kuwa, wakimbizi kutoka nchini Burundi wapo katika hatua ya kurejea kwao kutokana na hali ya amani na utulivu kutengemaa nchini humo.

Baadhi ya mabalozi na wadau wa nchi wa maendeleo wakiwa wamewasili Kigoma ili kutembelea kambi za wakimbizi