Joy FM

TADB kuwezesha wafugaji na wakulima mikopo Kigoma

22 September 2025, 12:23

Muonekano wa mayai yanayozalishwa ndani ya kiwanda cha Mayai Limited kilichopo Kaseke Wilaya Kigoma, Picha na Tryphone Odace

Wafugaji na wakulima wameomba Serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo kuendeleaa kuwapa mikopo ili waweze kuendesha shughuli zao na kuongeza thamani ya bidhaa wanazozalisha

Na Tryphone Odace

Benki ya Kilimo Tanzania TADB imesema inaendelea kufanya mapinduzi ya kilimo kwa kuwawezesha wakulima na wafugaji ili waweze kutoka kwenye kilimo cha kujimu na kufanya kilimo biashara ili kuongeza thamani ya mazao na uzalishaji wenye tija.

Afisa biashara kutoka Benki ya kilimo Tanzania Patrick Kafungu amesema hayo  wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea kiwanda cha Mayai Limited kilichopo kijiji cha Kaseke halmashauri ya Wilaya Kigoma ambacho kinajihusisha na uzalishaji wa mayai baada ya kupata uwezeshaji kutoka benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania.

Bw. Kafungu amesema lengo ni kuhakikisha wanawasaidia wakulima wadogo wadogo na wafugaji  ili waweze kuongeze thamani mazao yao ambapo kiwanda hicho kwa sasa kinaweza kuzalisha kreti za mayai ya kutosha jambo ambalo linatajwa kuwanufaisha.

Sauti ya Afisa biashara kutoka Benki ya kilimo Tanzania TADB, Patric Kafungu

Naye Mkurugenzi wa kiwanda cha Mayai Limited, Bw. Lupinda Sing Sundru amesema benki ya kilimo Tanzania TADB imeweza kuwapa asilimia 80 ya uwezeshaji na hivyo kuwainua na kuongeza uzalishaji kiwandani hapo.

Sauti ya Afisa biashara kutoka Benki ya kilimo Tanzania TADB, Patric Kafungu

Aidha ameongeza kuwa mradi huo mpaka sasa una kuku elfu tisini na mbili  na kuwa na uwezo kuzalisha kreti za mayai 3000 kwa siku na unatajwa kuongeza ajira kwa wananchi hasa wanaozunguka mradi huo.

Naye Mkurugenzi wa kiwanda cha Mayai Limited Lupinda Sing Sundru amesema benki ya kilimo tanzania TADB imeweza kuwaoa asilimia 80 ya uwezeshaji na hivyo kuwainua na kuongeza uzalishaji.

Aidha ameongeza kuwa mradi huo mpaka sasa una kuku elfu tisini na mbili na kuwa na uwezo kuzalisha kreti za mayai 3000 kwa siku na unatajwa kuongeza ajira kwa wananchi hasa wanaozunguka mradi huo.

Sauti ya Mkurugenzi wa kiwanda cha Mayai Limited Lupinda Sing Sundru
Mayai yanayozalishwa na kiwanda cha Mayai Limited yakiwa yamepangwa kwenye Kreti za mayai, Picha na Tryphone Odace

Baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho wameeleza namna wanavyofaika na kiwanda hicho na kuwa wameweza kuendesha maisha ya familia zao.

Wanufaika wa kiwanda cha Mayai Limited