Joy FM

ACT Wazalendo kuifanya Kagera kuwa eneo la kimkakati

18 September 2025, 10:09

Wananchi na wafuasi wa chama cha ACT Wazalendo wakiwa katika mkutano wa kampeni katika kata ya Kagera, Picha na Mwandishi wetu

Chama cha ACT Wazalendo kimeahidi kuhakikisha kinatatua changamoto zinawakabili wananchi wa Kata ya Kagera Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa kuboresha na kuendelea miradi iliyoanzishwa na chama hichi kwa kipindi walichokuwepo madarakani ikiwemo barabara na maji

Na Mwandishi wetu

Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo  Jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe amesema kuwa iwapo atachaguliwa kuwa mbunge atahakikisha anaanzisha mfumo wa hifadhi ya jamii kwa watu wote ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya pamoja na uboreshaji wa barabara na maji.

Akizungumza katika mkutano wa kampeni za chama hicho  na wananchi wa kata ya Kagera Manispaa ya Kigoma Ujiji, Zitto Kabwe amesema kumekuwepo na ukosefu huduma bora za afya na maji jambo ambalo linasababisha wananchi washindwe kufanya kazi kwa ufanisi.

Sauti ya Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo  Jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe
Mgombea ubunge Jimbo la Kigoma Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Zitto Kabwe akiwa katika kampeni Kata ya Kagera Manispaa ya Kigoma Ujiji, Picha na Mwandishi wetu

Amesema ili kurahisisha shughuli za usafirishaji kwa wananchi wa kata ya kagera watahakikisha wanajenga barabara na daraja.

Sauti ya Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo  Jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe

Aidha amesema kuwa watahakikisha wanaendeleza mradi wa umwagiliaji wa mto Luuiche ili uweze kuwanufaisha wananchi na kuifanya kata hiyo kuwa eneo la kimkakati.

Sauti ya Mgombea ubunge kwa tiketi ya chama cha ACT Wazalendo  Jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe

Baadhi ya wananchi wa kata ya kagera wameomba mgombea huyo wa Ubunge kuwasaidia kulipwa fidia kwa wananchi waliobomolewa nyumba zao na kuhakikisha anatatua changamoto ambazo zimekuwa zikiwakabili ikiwemo ukosefu wa vitambulisho vya Taifa NIDA na mikopo kwa vijana.

Wananchi na wafuasi wa chama cha ACT Wazalendo wakiwa katika mkutano wa kampeni katika kata ya Kagera, Picha na Mwandishi wetu

Chama cha ACT Wazalendo kinaendelea na kampeni katika maeneo mbalimbali na kueleza sera zake kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktaoba 29 mwaka huu.