Joy FM

NGOs zaaswa kuepuka utakatishaji fedha na ugaidi Kigoma

4 September 2025, 15:09

Baadhi ya viongozi wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali wakiwa na Katibu tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa, Picha na Tryphone Odace

Tanzania imekuwa mojawapo ya nchi zilizo Mashariki na Kusini mwa Afrika zilizopiga hatua kubwa katika udhibiti wa utakasishaji fedha haramu na uzuiaji wa silaha za maangamizi na ufadhili wa ugaidi nchini.

Na Tryphone Odace

Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali Mkoani Kigoma yametakiwa kuwa makini na kuepuka kutotumiwa vibaya watu wenye nia mbaya na kuingia katika kashfa za utakatishaji fedha haramu na ugaidi ili kusaidia kutoliingiza taifa katika migogoro na machafuko.

Katika ulimwengu wa leo, mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yanachukuliwa kama nguzo muhimu ya maendeleo ya kijamii, kiuchumi na hata kisiasa.

Hata hivyo, yapo baadhi ya mashirika yanayohusika au kutumiwa vibaya kwa shughuli haramu kama vile utakatishaji wa fedha na kufadhili ugaidi na vitendo hivi vinatajwa kuwa na  athari kubwa siyo tu kwa serikali bali pia kwa jamii nzima.

Washiriki wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali Mkoani Kigoma, Picha na Tryphone Odace

Akizungumza na viongozi wa dini na mashirka yasikuwa ya kiserikali Mkoani Kigoma, Wakili wa Serikali kutoka ofisi ya Waziri Mkuu, Julias Msengeli amesema utakatishaji wa fedha haramu na ugaidi kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali ni tishio kubwa kwa maendeleo ya taifa na ustawi wa jamii.

Sauti ya Wakili wa Serikali kutoka ofisi ya Waziri Mkuu, Julias Msengeli

Naye Kamishna Msaidizi kutoka kitengo cha fedha haramu Seif Omary Khaji amesema taasisi zisizo za kiserikali zimekuwa zikitumiwa na wahalifu na kupoteza lengo la kuanzishwa kwake ikiwemo kuhudumia jamii.

Sauti ya Kamishna Msaidizi kutoka kitengo cha fedha haramu Seif Omary Khaji

Katibu tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa anawakumbusha wamiliki wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kutambua wajibu wao ikiwmo kufuata sheria za mashirika hayo.

Sauti ya Katibu tawala Mkoa wa Kigoma Hassan Rugwa

Baadhi ya wadau wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali wameeleza umuhimu wa mafunzo hayo ili kuhakikisha hayawi sehemu ya uvunjifu wa sheria.

Sauti ya baadhi ya wadau wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali

Ni jukumu la serikali, vyombo vya usalama, jamii na mashirika yenyewe kuhakikisha kuwa taasisi hizi hazitumiki kama chombo cha uhalifu. Ufuatiliaji, uwazi, na ushirikiano wa kimataifa ni muhimu katika kupambana na changamoto hii hatarishi ya utakatishaji fedha na ugaidi.

Hata hivyo, Tanzania imetajwa kuondolewa kwenye Orodha ya nchi zenye mapungufu ya kimkakati katika mifumo ya udhibiti utakatishaji fedha haramu, ufadhili wa ugaidi, na ufadhili wa silaha za maangamizi.