Joy FM

RC Kigoma aingilia kati mgogoro wa ardhi mwekezaji na wananchi

3 September 2025, 08:49

Mkuu wa Mkoa Kigoma Balozi Simon Sirro akizungumza na wananchi wa Ruchugi Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma, Picha na Orida Sayon

Serikali Mkoani Kigoma imeanza kuchukua hatua kuhusu mgogoro wa eneo la hekta 10,000 ambalo wananchi wa kijiji cha Ruchugi wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma wanadaiwa kuvamia eneo la mwekezaji kampuni ya FAZENDA ambayo imekusudia kuwekeza katika mradi wa kilimo huku kutakiwa kuondoka ili mwekezaji aanze shughuli zake.

Na Orida Sayon

Zaidi ya wananchi 800 wanaoishi katika eneo la Ruchugi katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma wameomba serikali kuwapatia eneo la kuishi na kufanya shughuli za kilimo ili kupisha shughuli za uwekezaji katika eneo hilo.

Hayo yamejili katika mkutano kati ya wananchi na Mkuu wa wa Mkoa wa Kigoma IGP mstaafu Simon Nyakoo Sirro uliofanyika leo katika eneo la Ruchugi Wilayani Uvinza uliolenga kutoa maelekezo kuhusu kupisha eneo hilo kwa ajili ya uwekezaji.

Kwa mujibu wa mkutano uliofanyika mnamo mwezi August 2025 wananchi wanaofanya shughuli zao walipaswa kuhama eneo hilo ndani ya siku 14 .

Sauti ya wananchi Wilayani Uvinza

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Dinah Mathamani ambapo amesema eneo hilo ni miongoni mwa maeneo ya uwekezaji na Halmashauri imetekeleza sera ya serikali ya uwekezaji.

Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Dinah Mathamani, Picha na Orida Sayon
Sauti ya Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Dinah Mathamani

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma IGP mstaafu Simon Sirro ametamatisha mkutano huo kwa kutoa maelekezo kwa wananchi kuendelea na shughuli zao huku watendaji wakifanya mapitio na mwekezaji.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma IGP mstaafu Simon Sirro

Eneo hilo la uwekezaji lipo katika makao makuu ya Wilaya ya Uvinza ikichukua jumla na hekari elfu 10 likitarajiwa kufanyika uwekezaji wa kilimo na kampuni ya FAZENDA Tanzania Limited.