Joy FM

Serikali yazindua chumvi lishe ya mifugo Uvinza

18 August 2025, 08:49

Uzalishaji wa chumvi ukiwa unaendelea katika kiwanda cha chumvi cha Nyanza Mines, Picha na Tryphone Odace

Wafugaji wanatarajia kunufaika na uzalishaji wa chumvi lishe kwa ajili ya mifugo na kuongeza thamani ya mifugo na kunufaika na masoko ya ndani na nje ya nchi.

Na Tryphone Odace

Waziri wa Madini Anthony Mavunde amesema kuwa  hatua ya kiwanda cha chumvi cha Nyanza Mines kilichopo Wilayani Uvinza Mkoani Kigoma kuendelea kufanya maboresho ikiwemo upanuzi wa kiwanda hicho itasaidia kuongeza uzalishaji wa chumvi na kuacha kutegemea chumvi kutoka nje ya nchi.

Waziri Mavunde amesema hayo alipotembelea kiwanda cha Nyanza Mines kilichopo wilayani uvinza mkoani kigoma na kuzindua chumvi lishe kwa ajili ya mifugo na kuwa hatua hiyo itasaidia kuongeza kipato kwa Taifa.

Amesema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha inatumia rasilimali zilizopo na kuacha kutegemea  chumvi kutoka nje na kuwa kiwanda hicho kuanza kuzalisha chumvi lishe kwa ajili ya mifugo ni hatua kubwa na kuungwa mkono kwa manufaa ya mifugo nchini.

Sauti ya Waziri wa Madini Antony Mavunde
Muonekano wa kiwanda cha chumvi cha Nyanza Mines kilichpo Wilayani Uvinza, Picha na Tryphone Odace

Naye Mkuu wa Wilaya Uvinza Dinnah Mathamani amesema kupitia kiwanda hicho cha kuzalisha chumvi ya mifugo itachochea na kuongeza thamani ya mifugo na kuweza kuuzwa ndani na nje ya nchii.

Sauti ya Mkuu wa Wilaya Uvinza Dinnah Mathamani

Kwa upande wake, Ben Mwaipopo Mkurugenzi Mkaazi wa kiwanda cha Nyanza Mines amesema uboreshaji wa kiwanda hicho kumeongeza uzalishaji kutoka tani elfu 9 hadi tani elfu 75 kwa mwaka huu baada ya kufanyika kwa uwekezaji.

Sauti ya Ben Mwaipopo Mkurugenzi Mkaazi wa kiwanda cha Nyanza Mines