Joy FM

Serikali yatoa msamaha wa kodi kwa pikipiki

6 August 2025, 13:43

Maafisa kutoka TRA wakiwa katika kipindi cha Goodmorning Kigoma kinachorushwa na Redio Joy Fm, Picha na Mullovan Cheppa

Neema yawashukia wamiliki na madereva wa pikipiki baada ya Serikali kueleza kuwa imeondoa kodi kwa vyombo hivyo

Na Timotheo Leonard

Serikali imeondoa kodi ya mapato ya shilingi laki moja na elfu ishirini kwa mwaka kwa vyombo vya pikipiki maarufu kama bodaboda ili kuwapa fursa ya kuinua uchumi wao.

Hayo yamebainishwa na Hamad Iddy Mterry, Afisa Mkuu wa usimamizi wa kodi kutoka mamlaka ya mapata Tanzania TRA, wakati akizungumza na Redio Joy fm kuhusu mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi yaliyofanyika kupitia sheria ya fedha mwaka 2025

Amesema malengo ya serikali kutoa msamaha wa kodi hiyo kwa vyombo vya pikipiki ni kutaka kuwapa nafasi ya kukuza shughuli zao na kuwataka watendaji wa serikali kusimamia ipasavyo.

Sauti ya Hamad Iddy Mterry, Afisa Mkuu wa usimamizi wa kodi kutoka mamlaka ya mapata Tanzania TRA

Baadhi ya madereva wa pikipiki wa kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma Ujiji, wameishukuru serikali kwa kuondoa kodi hiyo huku wakisema itawasaidia kukua kiuchumi.

Sauti ya Baadhi ya madereva wa pikipiki wa kata ya Kibirizi

Aidha serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanya mabadiliko ya sheria mbalimbali za kodi yaliyofanyika kupitia sheria ya fedha mwaka 2025 ili kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato kwa maendeleo ya Taifa.