Joy FM
Joy FM
5 August 2025, 12:49

Wanawake kuwa viongozi inahitajika mikakati ya kina inayojumuisha elimu, fursa, mazingira wezeshi, na mabadiliko ya mitazamo ya kijamii ili waweze kusimama na kuweza kuongoza
Mkuu wa Wilaya ya Uvinza Dinah Mathamani amefunga mafunzo ya siku nne yaliyokuwa na lengo la kuwajengea uwezo wa kiuongozi wanawake ambao ni wakuu katika vitengo na idara kwa Halmashauri nane za mkoa wa Kigoma pamoja na sekretarieti ya Mkoa huku akiwasisitiza mabadiliko chanya katika kujitambua, ufanisi wa kazi, kulinda heshima yao na kuwa sehemu ya kuchochea maendeleo ya nchi huku wakimlinda mtoto wa kike.