Joy FM

Neema yawashukia wakulima wa kahawa Kasulu

24 July 2025, 15:30

Muonekano wa miche ya kahawa ikiwa kwenye kitalu, Picha na Emmanuel Kamangu

Halamshauri ya Wilaya Kasulu imepanga kuzalisha miche milioni moja  ya kahawa ili kutoa fursa kwa wakulima  wengi kufikiwa na kuongeza tija ya uzalishaji wa zao hilo.

Na Emmanuel Kamangu

Wakulima wa zao la kahawa katika kijiji cha Kibirizi kata ya Buhoro Halamshauri ya Wilaya ya Kasulu wameishukuru Serikali kwa kuwapatia  miche pamoja mbegu bora za kisasa za kahawa aina ya Arabica mbegu zinayotajwa kuwa bora tofauti na mbegu za zamani.

Baadhi ya  wakulima  hao akiwemo Bi. Lidia Kasimiri   wakizungumza na Redio Joy mara baada ya kutembelewa na Kaimu Mkuu idara ya Kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu kwa ajili ya  kuona maendeleo ya zao  la kahawa  katika kata ya Buhoro  wameishukuru Serikali  kwa kuwapatia  bure miche ya kisasa.

Baadhi ya wakulima wa Kahawa
Mwalimu Stanslaus Petro miongoni mwa wakulima wa Kahawa, Picha na Emmanuel Kamangu

Naye Mwalimu wa Taaluma  Shule ya Msingi Buhoro Bw. Stanslaus Petro amesema  kilimo cha zao la kahawa katika shule hiyo kimewasaidia sana  kuongeza kipato  cha shule na kupelekea  wanafunzi kupata uji shuleni hapo.

Sauti ya Mwalimu wa Taaluma  Shule ya Msingi Buhoro Bw. Stanslaus Petro

Kaimu Mkuu idara ya Kilimo katka halmashauri  hiyo   Bw. Masumbuko Kelemwa  akiwa katika ziara  hiyo ya kutembelea mashamba ya wakulima ya kahawa kata Buhoro    amesema ugawaji bure wa miche  ya kahawa aina ya Arabica umeleta matokeo chanya kwa kuongeza idadi ya wakulima kutoka 50 hadi kufikia 350 ndani ya mwaka mmoja na hii ikichangiwa na wakulima wengi  kuvutiwa na mbegu hiyo ambayo hustahimili magonjwa na kuzaa kwa wingi.

Sauti ya Kaimu Mkuu idara ya Kilimo katka halmashauri  hiyo   Bw. Masumbuko Kelemwa 
Kaimu Mkuu idara ya Kilimo halmashauri  ya Kasulu  Bw. Masumbuko Kelemwa  akiwa akiwa na wataalamu wengine wa kilimo, Picha na Emmanuel Kamangu