Joy FM

RC Kigoma ahimiza eneo la uwekezaji zao la muhogo

8 July 2025, 17:26

Mkuu wa Mkoa Kigoma akisalimia na viongozi na watumishi wa Halmashauri za Wilaya Kasulu, Picha na Josephine Kiravu

Mkoa wa Kigoma unaendelea kufanya vizuri kitaifa katika uzalishaji wa zao la Muhogo ambapo makadirio kwa mwaka hufikia  hadi tani milioni 1.2 za muhogo mkavu na mbichi huku matarajio ikiwa ni kufikia zaidi ya tani milioni 3 ifikapo mwaka 2030.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amezitaka Halmashauri za Wilaya Kasulu kutenga eneo kubwa la uwekezaji wa zao la kilimo cha muhogo ili kuleta mapinduzi makubwa ya uzalishaji kutokana na utayari wa wawekezaji kutoka china ambako kwa sasa soko la zao hilo ni kubwa.

Simulizi ya Jacob Ruvulo juu ya mkakati wa kutengwa eneo la uwekezaji kwa ajili ya zao la muhogo