Joy FM

Watakiwa kuliombea taifa kuelekea uchaguzi mkuu

26 May 2025, 16:18

Askofu wa Dayosisi ya Western Tanganyika Mhashamu Emmanuel Bwatta, Picha na Hagai Ruyagila

Wakati Taifa likeelekea katika uchaguzi Mkuu, wakristo wameaswa kuendelea kuombea amani

Na Hagai Ruyagila

Waumini wa Dini ya Kikristo wilayani Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kuliombea taifa kuelekea katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi ocktoba mwaka huu ili ufanyike kwa amani na utulivu.

Akizungumza kwenye ibada takatifu ya ufunguzi wa kanisa la Anglikan Dinal ya Mwilamvya, Askofu wa Dayosisi ya Western Tanganyika Mhashamu Emmanuel Bwatta amesema waumini pamoja na viongozi wa dini wanapaswa kutumia majukwaa yao kuliombea taifa ili uchaguzi Mkuu mwaka huu ufanyike kwa amani.

Sauti ya Askofu wa Dayosisi ya Western Tanganyika Mhashamu Emmanuel Bwatta

Aidha Askofu Bwatta amepiga marufuku viongozi wa vyama vya siasa kufanya kampeni za uchguzi katika nyumba za ibada.

Sauti ya Askofu wa Dayosisi ya Western Tanganyika Mhashamu Emmanuel Bwatta

Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanal Isaac Mwakisu amesema kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya imejipanga kuhakikisha inaimarisha ulinzi na usalama huku akitoa wito kwa waumini kuendelea kuomba amani kabla na baada ya uchaguzi mkuu.

Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanal Isaac Mwakisu, Picha na Hagai Ruyagila
Sauti ya Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanal Isaac Mwakisu

Baadhi ya Waumini wa kanisa la Anglikana Mwilamvya wamesema niwajibu wao kuliombea amani taifa ili jamii iweze kuishi kwa upendo umoja na mshikamano.

Sauti ya Baadhi ya Waumini wa kanisa la Anglikana Mwilamvya
Baadhi ya Waumini katika ibada ya ufunguzi wa kanisa la Anglikana Dinal ya mwilamvya, Picha na Hagai Ruyagila