Joy FM

RC Kigoma ataka wajiri na waajiriwa kuzingatia haki na usawa

2 May 2025, 13:05

Wafanyakazi kutoka sekta mbalimbali wakiwa katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi yaliyofanyika Wilayani Kakonko, Picha na Hagai Ruyagila

Mratibu wa shirikisho wa vyama vya wafanyakazi ameomba Serikali kufanyia marekebisho sheria ya utumishi wa umma ili kuondoa mkanganyiko.

Na Hagai Ruyagila – Kakonko

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, amevitaka vyama vya wafanyakazi kuhakikisha vinazingatia usawa wa haki baina ya waajiri na waajiriwa ili kupunguza migogoro sehemu za kazi.

Andengenye ametoa wito huo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Mwenge, wilayani Kakonko, mkoani Kigoma.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye, Picha na Hagai Ruyagila

Amesema ni muhimu kwa vyama vya wafanyakazi kutekeleza majukumu yao kwa haki na usawa bila kupendelea upande wowote, ili kulinda amani na ustawi katika mazingira ya kazi.

Sauti ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye

Kwa upande wake, Mratibu wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi mkoani Kigoma Jumanne Magulu ameieleza serikali katika risala kuhusu changamoto zinazokabili wafanyakazi na kuiomba kufanya marekebisho ya sheria ya utumishi wa umma ili kuondoa mkanganyiko uliopo kati yake na sheria ya ajira na mahusiano kazini.

Sauti ya Mratibu wa Shirikisho la vyama vya wafanyakazi mkoani Kigoma Jumanne Magulu
Pichani ni baadhi ya wafanyakazi wakiwa katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi iliyofanyika Wilayani Kakonko, Picha na Hagai Ruyagila

Baadhi ya wafanyakazi waliotoa maoni yao wamesisitiza umuhimu wa uwajibikaji kazini ili kuchochea maendeleo katika maeneo yao ya kazi.

Sauti ya Baadhi ya wafanyakazi

Maadhimisho ya mwaka huu ya siku ya wafanyakazi Meimosi yamebeba kaulimbiu isemayo uchaguzi mkuu 2025 utuletee viongozi wanaojali haki na maslahi ya wafanyakazi sote tushiriki.