Joy FM

Wadau wa uchaguzi wapitisha muhtasari wa tume jimbo kugawanywa

24 April 2025, 12:33

Muonekano wa logo ya Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi, Picha na Tovuti ya tume

Tume huru ya Taifa imeendelea kusimamia ugawanyaji wa majimbo yalikuwa yanaonekana makubwa na hivyo kugawanywa ili kuweza kusogeza huduma kwa wananchi

Na Lucaa Hoha

Wadau wa uchaguzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma wamepitisha muhtasari kutoka tume huru ya Taifa ya uchaguzi kuhusu mapendekezo yaliyowasilishwa na wananchi ya kuligawa jimbo la kasulu Vijijini lengo likiwa ni kusogeza huduma za kijamii karibu na wananchi.

Nathanael Ndelema ni Diwani wa Kata ya Nyamyusi akizungumza kwa niaba wa wadau hao wa uchaguzi kwenye kikao kilichowakutanisha viongozi mbalimbali akiwemo mwakilishi wa mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Michael Ngayalina.

Sauti ya Nathanael Ndelema ni Diwani wa Kata ya Nyamyusi

Awali mkurugenzi wa huduma za sheria ya tume huru ya Taifa ya uchaguzi Mtibora selemani ambaye amemwakilisha Mkurugenzi wa tume huru ya Taifa ya uchaguzi ametaja majina mapya ya jimbo na kata zitakazounda jimbo hilo pindi watakapoligawa jimbo la Kasulu vijijini

Sauti ya Mkurugenzi wa huduma za sheria ya tume huru ya Taifa ya uchaguzi Mtibora selemani

Hamza Selemani ni    Mwakilishi wa mjumbe wa tume huru ya Taifa ya uchaguzi amesema kwa mjibu wa ibara ya 75 kifungu kidogo cha 4 na 74 kifungu kidogo cha 6C za katiba ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977  ikisomwa pamoja na kifungu cha 10 kifungu  kidogo cha 1D cha sheria ya tume huru ya taifa ya uchaguzi 1 ya mwaka 2024 tume  ina jukumu la kuchunguza na kuigawa jamhuri ya muungano katika majimbo ya uchaguzi.

Sauti ta Hamza Selemani ni    Mwakilishi wa mjumbe wa tume huru ya Taifa ya uchaguzi